Saturday, December 20, 2014

UBATIZO KAMA UNAVYOFUNDISHWA NA BIBILIA.

 
 
UBATIZO KAMA UNAVYOFUNDISHWA NA BIBILIA.
Nimeona ni vema nichukue muda wangu kidogo kuandika juu ya somo hili nyeti ambalo limekuwa sababu ya mvutano mkubwa sana katika mwili wa Yesu Kristo hususa katika nchi yetu.
Binafsi ninapozungumzia mwili wa Yesu Kristo nazungumzia kila mmoja ambaye amesafishwa na damu ya Yesu Kristo na kufanya uamuzi wa kumpa Yesu maisha yake kwa njia ya kuokoka. Mwili wa Yesu Kristo haujumuishwi na madhehebu ya Kikristo yaliyopo bali na watu toka madhehebu hayo yote ambao wameoshwa dhambi zao kwa damu ya Yesu baada ya kufanya maamuzi ya kumpa Yesu maisha yao, yaani wameokoka au wamezaliwa mara ya pili. Mwongozo thabiti wa watu hawa sio misimamo ya madhehebu wanayotoka bali ni neno la Mungu na ndicho kinachotuunganisha wanamwili wa Kristo bila kujali tumetoka madhehebu gani. Kwa kuwa kila dhehebu, kanisa na huduma lina utaratibu wake wenyewe kiunganishi kikuu cha watu wa Mungu toka madhehebu haya ni neno la Mungu ambalo pia linajulikana kama Bibilia au Maandiko Matakatifu.
Sasa ni dhahiri nikisema hivyo kwamba kila kanisa, huduma na dhehebu, lina utaratibu wake wa kubatiza. Wengine wana batiza watoto, wengie kwa maji machache, wengine kwa maji mengi nk. Nia ya fundisho hili sio kuingilia taratibu za makanisa, huduma au madhehebu za kubatiza bali ni kuleta ufahamu juu ya ubatizo ambao Yesu aliuagiza ambao huo hauna uhusiano hata kidogo na batizo zingine za kimapokeo ambazo zinaendelea katika makanisa, madhehebu au huduma mbalimbali.
Kila ubatizo upo kwa sababu zake na kwa makusudi yake. Ni wajibu wangu katika somo hili kufundisha ule ambao uliagizwa na Yesu.
UBATIZO NI NINI?
Neno ubatizo kama linavyotumika katika maandiko ya Agano Jipya linamaanisha kuzamisha ndani ya, linamaanisha kuzika katika, linamaanisha kufunika kabisa na.
Tukianzia kwenye maana ya neno ubatizo na jinsi ambavyo limetumika katika bibilia hakuna kiashiria chochote kwamba hili zoezi linaweza likafanywa kwa kunyunyiza au kuogesha na maji. Ni wazi tukianzia kwenye maana hili zoezi katika utekelezaji wake litahitaji tu maji mengi ili kulikamilisha. Kwa hiyo ubatizo ni wa maji mengi na mhusika lazima azamishwe kabisa ndani ya maji hayo, afunikwe kabisa na hayo maji na azikwe kabisa ndani ya hayo maji.
Tunavyoendelea kutafakari hili somo kimaandiko tutazidi kuona kweli hii ikijidhihirisha tena na tena na tena katika maandiko na tutaona kabisa kuwa ubatizo aliyouagiza Yesu ni wa maji tele na huu hauna uhusiano kabisa na batizo za kimapokeo ambazo baadhi ya makanisa na madhehebu ya Kikristo wanatumia kuwathibitisha waumini wao.
Hii itatusaidia kama mwili wa Kristo kujua kuwa tukishamwamini Bwana Yesu na kuamua kuokoka inatupasa kubatizwa kwa ubatizo huu aliyouagiza hata kama awali kabla ya kuamini tulibatizwa katika madhehebu yetu, maana ule ubatizo tuliyobatizwa katika madhehebu yetu kabla ya kumwamini Yesu na kumfanya Bwana na Mwokozi wa Maisha Yetu una maana yake na huu aliyoagiza Yesu nao una maana na umuhimu wake.
MAANDIKO YANAFUNDISHA NINI KUHUSU UBATIZO?
Tuanze mjadala katika kipengele hiki kwa andiko la muhimu sana katika kuuanzisha mjadala huu na somo hili.
Waebrania 6: 1 - 3.
Kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu, na wa mafundisho ya mabatizo, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele. Na hayo tutafanya Mungu akitujalia. (EBR. 6:1-3 SUV).
Kwa mujibu wa hili andiko ubatizo miongoni mwa mafundisho mengine ni fundisho la kwanza au la msingi katika Ukristo. Msingi ni wa muhimu sana na ndiyo unaobeba jengo zima. Msingi ukiwekwa vibaya jengo linalokuja kujengwa juu yake hautakuwa na uhakika wa uimara.
Kwa kuwa ubatizo ni somo la msingi kulipuuzia na kulifanya halina umuhimu ni kosa kubwa sana kwa mujibu wa hili andiko. Kusema kuwa ukibatizwa na maji mengi au machache yote yatakauka ni kudharau mafundisho na maagizo ya Yesu juu ya hili na ni kupuuza na kubeza agizo la muhimu sana ambalo lilitolewa na Yesu Kristo. Umuhimu wa ubatizo sio kama unakauka au hukauki ni nani aliagiza ifanyike na iliagizwa ifanyike kwa utaratibu gani?
Kwa kuwa ubatizo ni moja ya maagizo ya msingi ya Yesu Kristo kwa kanisa kama tukipuuza hili agizo tutakuwa tumepuuza kitu cha muhimu sana ambacho kitasababisha msingi wa maisha yetu ya Ukristo kutokuwa kamili na kama Daudi alivyosema:
Zaburi 11: 3;
Kama misingi ikiharibika, Mwenye haki atafanya nini? (ZAB. 11:3 SUV).
Umuhimu mkubwa sana wa ubatizo unaenda tena kujidhihirisha katika maandiko haya yafuatayo:
I Yohana 5: 8, 9.
Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja. Kisha wako watatu washuhudiao duniani], Roho, na maji, na damu; na watatu hawa hupatana kwa habari moja. Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia Mwanawe. (1 YOH. 5:8, 9 SUV).
Mbinguni kuna watatu watakaotushuhudia na duniani pia kuna watatu watakaotushuhudia.
Kwa mbinguni watakuwa, Baba, Neno ambaye ni Yesu Kristo na Roho Mtakatifu.
Duniani napo kutakuwa na watatu, Roho Mtakatifu, maji na Damu.
Roho Mtakatifu atakushuhudia kuwa amekujaza. Maji yatakushuhudia kuwa yalikubatiza na Damu itakushuhudia kuwa ilikuosha.
Usipuuzie swala la ubatizo. Najua umeoshwa kwa Damu ya Yesu, umejazwa na Roho Mtakatifu, lakini je, umebatizwa baada ya kuamini na tena kama maandiko yanavyofundisha kwa maji mengi?
Kama kuna mtu mmoja ambaye alikuwa hana ulazima wa kubatizwa, alikuwa ni Yesu Kristo maana katika siku Zake, ubatizo uliyokuwepo, yaani ule wa Yohana ulikuwa ni ubatizo wa toba. Watu walikuja kwa Yohana Mbatizaji kubatizwa, wakizitubia dhambi zao.
Mathayo 3: 5, 6.
Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani; naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao. (MT. 3:5, 6 SUV).
Kama watu walikuwa wanakuja kwa Yohana Mbatizaji kubatizwa huku wakizitubia dhambi zao, na ubatizo wa Yohana ulikuwa wa toba, kulikuwa na umuhimu gani wa Yesu Kubatizwa wakati Yeye alikuwa Mwana Kondoo wa Mungu azichukuaye dhambi za ulimwengu? Asiye na dhambi anahitaji vipi kubatizwa ubatizo wa toba?
Pia kwenye huo mstari hapo juu natamani uone kuwa walibatizwa huku wakiziungama dhambi zao. Kwamba umeongozwa sala ya toba haimaanishi usibatizwe, ungama na kubatizwa mpendwa wangu, ndo utaratibu wa kibibilia.
Yohana Mbatizaji alilijua hilo kuhusu Yesu na ndo maana Yesu alipokuja kwa Yohana kubatizwa, Yohana alikataa kumbatiza maana hakuona kwanini ililazimu Yesu kubatizwa. Kimsingi kwa mantiki ya ubatizo wa Yohana, Yesu hakuwa na ulazima wowote wa kubatizwa kwa ubatizo huo lakini bado hata hivyo alibatizwa.
Mathayo 3: 13 - 15.
Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe. Lakini Yohana alitaka kumzuia, akisema, Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu? Yesu akajibu akamwambia, Kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Basi akamkubali. (MT. 3:13-15 SUV).
Ona maneno ambayo Yesu aliyasema, kubali hivi sasa, ndivyo ITUPASAVYO kutimiza haki yote.
Neno ITUPASAVYO ni neno la ufunguo sana katika huu mstari. Yesu hakusema INIPASAVYO, alisema ITUPASAVYO. Kila mmoja wetu inatupasa kubatizwa. Kama Yesu ambaye hakuhitaji kubatizwa alibatizwa mimi na wewe ni nani tujihesabie haki na kuona hatuwezi wala hatuhitaji kubatizwa?
Kama Yesu alitimiza haki yote kwa njia ya ubatizo, mimi na wewe ni nani tusiitimize haki yote pia kwa njia hiyo hiyo ya ubatizo?
Mtume Yohana katika waraka wake anazungumza jambo la muhimu na msingi sana.
I Yohana 2: 6.
Yeye asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama yeye alivyoenenda. (1 YOH. 2:6 SUV).
Kama tunadai kuwa tunakaa ndani Yake basi imetupasa kuenenda kama Yeye alivyo enenda. Kama Yesu alibatizwa na tena kwenye maji mengi basi imetupasa nasi pia kubatizwa kama Yeye na tena katika maji mengi.
Mtume Petro kwenye waraka wake naye anafundisha:
I Petro 2: 21.
Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake. (1 PET. 2:21 SUV).
Yesu alituachia kielelezo tufuate nyayo zake. Kama alibatizwa nasi tufuate kielelezo chake na tubatizwe pia.
Pia Mtume Petro anasema tena katika waraka wake:
I Petro 3: 21.
Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo. (1 PET. 3:21 SUV).
Haya maneno ya huyu mtume ni ya kina sana na ni muhimu yakizingatiwa. Anasema ubatizo unatuokoa siku hizi ila anakuwa makini sana kulisema kwa kina ili tusije tukaelewa vibaya tukafikiri ubatizo unaweza kuchukua nafasi ya Roho na Damu kama tulivyoona hapo awali. Ubatizo hauweki mbali uchafu wa mwili, hiyo ni kazi ya Damu ya Yesu, bali ni jibu la dhamiri safi mbele za Mungu. Kwa hiyo kusema kuwa ubatizo unatuokoa, anamaanisha kuwa una sehemu katika mchakato mzima wa wokovu wetu, ila sehemu yake kubwa ni kutupa jibu la dhamiri safi mbele za Mungu. Ndiyo maana kwa kila mmoja ambaye hajabatizwa baada ya kuamini na tena kwa maji tele, kila hili somo likizungumzwa, kujadiliwa, kufundishwa mbele zake anasikia dhamiri ikimchoma, maana hakuna namna mtu unaweza ukalipotezea jambo la muhimu kama hili, labda uamue tu kuchomwa dhamiri, usisikie tena.
Yesu alipokuwa anazungumza na Nikodemo kwa habari ya kuzaliwa mara ya pili, alisema maneno haya ambayo nayo ni ya muhimu sana kuzingatia:
Yohana 3: 3 - 5.
Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu. Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa? Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu. (YN. 3:3-5 SUV).
Yesu alikuwa anazungumza na Nikodemo kwa habari ya kuzaliwa mara ya pili na akamwambia wazi kabisa kuwa kuzaliwa mara ya pili ni kwa Roho na kwa maji.
Umezaliwa kwa Roho sawa, kwa maji je? Maana vyote viwili vinatakiwa ili kukamilisha kuzaliwa kwako mara ya pili na hapa Yesu dhahiri alipokuwa anazungumzia kuzaliwa kwa maji alikuwa anazungumza kuhusu ubatizo.
Haki ya Mungu inakiriwa kwa njia ya ubatizo na kupingwa kwa njia ya kukataa kubatizwa.
Luka 7: 29, 30.
Na watu wote na watoza ushuru waliposikia hayo, waliikiri haki ya Mungu, kwa kuwa wamebatizwa kwa ubatizo wa Yohana. Lakini, Mafarisayo na wana-sheria walilipinga shauri la Mungu juu yao, kwa kuwa hawakubatizwa naye. (LK. 7:29, 30 SUV).
Ishara ya nje kuwa wote na watoza ushuru wameikiri haki ya Mungu ni kule kukubali kwao kubatizwa ubatizo wa Yohana. Ila Mafarisayo na wana-sheria walilipinga shauri la Mungu juu yao kwa kuwa hawakubatizwa naye. Je wewe umeikiri haki ya Mungu kwa kubatizwa kwa ubatizo aliyoagiza Yesu au wewe ni miongoni mwao wanaopinga shauri la Mungu juu yao kwa kukataa kubatizwa. Jihoji, pata jibu alafu chukua hatua.
Ili kujua kuwa ubatizo ulikuwa wa muhimu kiasi gani, sio tu Yohana ambaye alikuwa anabatiza lakini hata Yesu alipoianza huduma Yake akihubiri habari za Ufalme wa Mungu na toba, naye pia alikuwa anabatiza.
Yohana 3: 23, 26.
Baada ya hayo Yesu na wanafunzi wake walikwenda mpaka nchi ya Uyahudi; akashinda huko pamoja nao, akabatiza. Wakamwendea Yohana, wakamwambia, Rabi, yeye aliyekuwa pamoja nawe ng’ambo ya Yordani, yeye uliyemshuhudia, tazama, huyo anabatiza na watu wote wanamwendea. (YN. 3:22, 26 SUV).
Yesu ni dhahiri kwa maandiko hayo hapo juu alikuwa akibatiza. Alienda Uyahudi na wanafunzi Wake, akashinda huko akibatiza. Kama ubatizo hauna umuhimu kiviile, Yesu anaendaje kushinda mahali akifanya zoezi ambalo halina umuhimu?
Aliyeshuhudiwa na Yohana Mbatizaji ng'ambo ya Yordani ni nani kama sio Yesu? Na hapa imeandikwa alikuwa anabatiza na wote walikuwa wakimwendea.
Kama Yesu alikuwa akibatiza mimi na wewe ni nani kusema kuwa sisi hatubatizi au kupinga ubatizo?
Yohana 4: 1, 2.
Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza, (lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake,) (YN. 4:1, 2 SUV).
Hili andiko latuonyesha kuwa Yesu mwenyewe binafsi hakuwa anabatiza bali wanafunzi wake ikimaanisha wazi kuwa walifundishwa na Yesu kubatiza. Ni huku kubatiza kulikuwa mchakato wa muhimu sana katika kuwafanya watu wanafunzi. Yesu alikasimu wajibu wa kubatiza kwa wanafunzi Wake, ili Yeye asije akajichosha kwa kufundisha, kufanya huduma kwa wagonjwa na waliyofungwa na juu yake kubatiza maelfu ya watu waliyokuwa wanamjia.
Yesu kwenye huduma Yake alibatiza, je mimi na wewe tunaweza kuwa zaidi Yake Yeye au tutafuata mfano Wake wa Kihuduma?
Tunafahamu kuwa Yohana Mbatizaji pia alipokuwa anabatiza watu aliwabatizia mto Yordani maana maji mengi yanahitajika kwa ajili ya kufanikisha na kukamilisha zoezi la ubatizo kibibilia.
Alionekana tena akibatiza watu mahali pengine na mahali hapo pengine palichaguliwa kama mahali pa kubatizia kwa kuwa kulikuwa na maji tele.
Yohana 3: 23.
Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni, karibu na Salimu, kwa sababu huko kulikuwa na maji tele; na watu wakamwendea, wakabatizwa. (YN. 3:23 SUV).
Ni dhahiri kabisa kwamba ubatizo ni kwa maji mengi na sio kwa kunyunyizwa, japo mimi sipingi ubatizo wa kunyunyizwa, ila sio uliyoagizwa na bibilia.
Katika mfano wa towashi wa Kushi, tunaona tena kuwa ubatizo ulikuwa ni wa maji tele sio wa kunyunyizwa.
Matendo 8: 36 - 39.
Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? [ Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.] Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza. (MDO 8:36-38 SUV).
Kama njiani walifika mahali penye maji, haya maji lazima yalikuwa tele na walipoyaona au towashi alipoyaona, akasema maji haya hapa nini kinanizuia nisibatizwe. Akaambiwa ukiamini kwa moyo wako wote inawezekana. Hii ni dhahiri kuwa hili tendo la ubatizo linafanywa baada ya mtu kuamini kwa moyo wake wote na sio kuna mtu anaamini kwa niaba yake. Kwa hiyo ubatizo wa watoto wafogo wasio na uwezo wa kuamini sio wa kibibilia hata kidogo na hata utaratibu wa baba na mama wa ubatizo sio wa kibibilia pia. Ni utaratibu tu wa kimapokeo katika makanisa yetu ambao mimi siupingi, ninasema una makusudi yake, sababu zake, madhumuni yake na malengo yake ila usichukuliwe kama mbadala wa ubatizo ambao Yesu aliuagiza au unaofundishwa na neno la Mungu. Tunaendelea kusoma towashi akikiri kuwa anaamini kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, wakateremka wote wawili majini ambayo ni kiashiria kuwa hayo maji yalikuwa mengi, akabatizwa.
Ili kutambua kuwa ubatizo sio jambo la kufanya nao mzaha, ubatizo ni msingi mmojawapo wa agizo la Yesu. Kama Yesu aliona umuhimu wa kutoa agizo mahususi la kuweka ubatizo kama sehemu ya kutimiza wito mkuu au agizo Lake kuu kwetu, hatutakuwa tunaitendea haki hilo agizo tunapokuwa tunapuuzia swala la ubatizo.
Mathayo 28: 19, 20.
Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari. (MT. 28:19, 20 SUV).
Agizo la Yesu la kuwafanya watu kuwa wanafunzi lina sehemu mbili, la kwanza likiwa kuwabatiza kwa Jina la Baba, na la Mwana na la Roho Mtakatifu, na la pili likiwa kuwafundisha kuyashika yote aliyotuamuru.
Hakuna namna unaweza kutimiza agizo kuu la Yesu bila ya kubatiza watu kama sehemu ya agizo hilo na hakuna namna unaweza kuwa mwanafunzi wa Yesu bila ya kubatizwa.
Yesu alisema maneno haya kuhusiana na mwanafunzi:
Mathayo 10: 24, 25.
Mwanafunzi hampiti mwalimu wake, wala mtumwa hampiti bwana wake. Yamtosha mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumwa kuwa kama bwana wake. Ikiwa wamemwita mwenye nyumba Beelzebuli, je! Si zaidi wale walio wa nyumbani mwake? (MT. 10:24, 25 SUV).
Mwanafunzi hawezi kuwa zaidi ya Mwalimu wake. Yatosha mwanafunzi kuwa kama Mwalimu wake. Sisi kam wanafunzi wa Yesu, kama Yesu alibatizwa na alifundisha tubatizwe, sisi ni nani kutobatizwa au kuzuia watu wasibatize?
Lakini pia msisitizo unawekwa tena kwenye nukuu ya Marko ya agizo ambalo Yesu alilitoa kwa wanafunzi Wake:
Marko 16: 15, 16.
Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. (MK. 16:15, 16 SUV).
Hivi maandiko yanaweza yakawa wazi zaidi ya hapa?
Tukaihubiri injili kwa kila kiumbe aaminiye na kubatizwa ataokoka, asiyeamini atahukumiwa. Umeamini nini kinakuzuia usibatizwe? Je ni mafundisho ya kidhehebu au ya kidini? Je ni mapokeo ya kidhehebu ndo yanakuzuia usibatizwe? Nakusihi kwa Jina la Bwana, pondeka nyenyekea ukabatizwe. Ni muhimu sana kuzingatia na kutii agizo la Yesu.
Umeamini moyoni mwako, umekiri kwa kinywa chako sasa kabatizwe ili kukamilisha mchakato mzima wa kuzaliwa kwako mara ya pili, ya kuokoka kwako.
Siku ya Pentekoste, Roho Mtakatifu alipolishukia kanisa kwa mara ya kwanza, Petro baada ya kuhubiri ujumbe moto moto wa Injili, watu walichomwa mioyo. Tunasoma:
Matendo 2: 37 - 42.
Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie. Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi. Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali. (MDO 2:37-42 SUV).
Walipochomwa mioyo na ujumbe wakauliza wafanyaje, wakaambiwa watubu wakabatizwe kila moja wao kwa Jina la Yesu. Nataka uone hayo maneno, KILA MOJA, maana agizo hili ni kwa ajili ya kila mmoja wetu. Sote twatakiwa kubatizwa baada ya kuamini. Tunaendelea kusoma kuwa wale waliyolipokea neno lake walibatizwa. Wewe ushalipokea neno kwanini unakuwa mbishi kubatizwa? Au hujalipokea nini? Baada ya kubatizwa wakadumu katika fundisho la mitume kama Yesu alivyoagiza, batizeni alafu fundisheni. Sasa mbona wewe unaruka hatua muhimu? Umeamini alafu sasa unadumu katika mafundiaho bila ya kubatizwa. Haijakaa sawa hiyo.
Yule mkuu wa gereza la Filipi naye alitaka kujua yale yampasayo ili naye aokoke na alipopewa maelekezo tunaona naye na nyumba yake wote walibatizwa.
Matendo 16: 30 - 33.
kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako. Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake. Akawakaribisha saa ile ile ya usiku, akawaosha mapigo yao, kisha akabatizwa, yeye na watu wake wote wakati uo huo. (MDO 16:30-33 SUV).
Wakati Petro alipokuwa yupo nyumbani kwa Cornelio akiwapelekea habari njema za wokovu wa Yesu, akiwa bado angali anahubiri walijazwa Roho Mtakatifu kwa ishara ya kunena kwa lugha mpya. Kilichofuata kinaonyesh umuhimu mkubwa ambao mitume waliweka kwenye swala zima la ubatizo na kwamba ubatizo sio kitu cha kupuuza na kuchukulia kiuwepesi.
Matendo 10: 44 - 48.
Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno. Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu, Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi? Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha. (MDO 10:44-48 SUV).
Ndugu yangu, wewe unakataa kubatizwa kwa sababu tu umeshajazwa Roho Mtakatifu? Damu imekutakasa, Roho amekujaza, kwanini na maji yasikubatize?
Kama ulishawahi kubatizwa kwa utaratibu wa kanisa au dhehebu lako kabla ya kuamini haimaanishi usibatizwe baada ya kuamini. Soma pamoja nami mkasa huu ufuatao.
Matendo 19: 1 - 5.
Ikawa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo, akiisha kupita kati ya nchi za juu, akafika Efeso; akakutana na wanafunzi kadha wa kadha huko; akawauliza, Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini? Wakamjibu, La, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia. Akawauliza, Basi mlibatizwa kwa ubatizo gani? Wakasema, Kwa ubatizo wa Yohana. Paulo akasema, Yohana alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani, Yesu. Waliposikia haya wakabatizwa kwa jina la Bwana Yesu. (MDO 19:1-5 SUV).
Alifika Efeso akakuta walikuwa wameshabatizwa kwa ubatizo wa Yohana. Paulo hakuupinga alianisha tu dhumuni la ubatizo ule akawafundisha ule uliyoagizwa na Yesu na walipoelewa wala hawakubisha kubatizwa "tena" maana walielewa ule waliyobatizwa ulikuwa wa dhumuni gani na huu wa baada ya kuamini habari za Yesu una dhumuni gani. Tusikwepe ubatizo kwa mafundisho manyonge yasiyo na mzizi katika neno la Mungu.
Najua ulishabatizwaga ubatizo wa kanisani kwako ulipokuwa mtoto, hujaamini bado, ule una sababu yake ila sio huu ambao Yesu na bibilia wanaufundisha ambao mtu anabatizwa baada ya kuokoka.
Hili andiko lifuatalo labda linaweza kutufungua tuelewe vema:
I Wakorintho 10: 1, 2.
Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari; (1 KOR. 10:1, 2 SUV).
Kama ambavyo wana wa Israel walibatizwa wawe wa Musa, tunaweza kubatizwa kuwa wa dhehebu fulani na pia tunaweza kubatizwa kuwa wa Yesu. Tusichanganye haya mambo.
Pia kuna watu nimeshawahi kuwasikia wakipinga swala la ubatizo kwa kusema Paulo alisema kuwa hakutumwa kubatiza.
Kwanza kabisa Paulo mwenyewe alibatizwa na Anania.
Matendo 9: 17, 18.
Anania akaenda zake, akaingia mle nyumbani; akamwekea mikono akisema, Ndugu Sauli, Bwana amenituma, Yesu, yeye aliyekutokea katika njia uliyoijia, upate kuona tena, ukajazwe Roho Mtakatifu. Mara vikaanguka machoni pake vitu kama magamba, akapata kuona, akasimama, akabatizwa; (MDO 9:17, 18 SUV).
Pili Paulo naye alibatiza.
Nashukuru, kwa sababu sikumbatiza mtu kwenu, ila Krispo na Gayo; Tena naliwabatiza watu wa nyumbani mwa Stefana; zaidi ya hao, sijui kama nalimbatiza mtu ye yote mwingine. (1 KOR. 1:14, 16 SUV).
Tunaona watu zaidi ya watatu hapa walibatizwa na Paulo mwenyewe, Krispo, Gayo na wa nyumbani mwa Stefana ambao hatuambiwi walikuwa wangapi alafu anamalizia kwa kusema zaidi ya hao sijui kama nilibatiza ye yote mwingine. Hakusema hakubatiza mwingine ni kwamba tu hakumbuki kama alibatiza mwingine. Na ndipo anasema hakutumwa yeye kubatiza.
I Korintho 1: 17.
Maana Kristo hakunituma ili nibatize, bali niihubiri Habari Njema; wala si kwa hekima ya maneno, msalaba wa Kristo usije ukabatilika. (1 KOR. 1:17 SUV).
Kusema hivi haikumaanisha ubatizo ni mbaya au sio lazima bali ubatizo haukuwa sehemu ya msisitizo wa huduma ya Paulo.
Jambo la tatu ni kwamba kwenye agano jipya sijamwona mtu ambaye anafundisha kwa undani ubatizo na maana na faida zake kama Paulo kwenye nyaraka zake.
Kwa hayo tuliyoyapitia kwenye maandiko ni wazi kabisa ubatizo ni jambo lisilo kwepeka wala kuepukika.
NINI FAIDA NA UMUHIMU WA KUBATIZWA?
Ningependa sasa kumalizia somo langu hili na mafundisho yangu haya kwa kuangalia umuhimu na faida za kubatizwa na hapa tutaweka mkazo kwa kutumia maandiko kutoka katika nyaraka za mtume Paulo.
Warumi 6: 3 - 5.
Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima. Kwa maana kama mlivyounganika naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika mtaunganika kwa mfano wa kufufuka kwake; (RUM. 6:3-5 SUV).
Tunapobatizwa katika Kristo Yesu tunabatizwa katika mauti Yake. Tunapozamishwa ndani ya maji mengi ni ishara ya kuzikwa pamoja na Kristo katika mauti Yake, ili tunapotoka sasa kwenye hayo maji iwe ni ishara ya kuingia katika upya wa uzima kama ambavyo Yesu Naye alifufukuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba. Kubatizwa kunatuunganisha na mfano wa mauti Yake, ili tuje tuunganike Naye katika mfano wa kufufuka Kwake.
Kolosai 2: 12.
Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu. (KOL. 2:12 SUV).
Tunapobatizwa tunazikwa pamoja Naye katika ubatizo. Kila ambaye hajabatizwa hajazikwa pamoja Naye na kwanini upuuzie kitu cha muhimu hivi? Anaendelea kusema katika huo tumefufuliwa pamoja naye, katika huo nini? Ubatizo ndugu yangu, kwa kuamini nguvu za Mungu aliyemfugua katika wafu.
Kitendo cha kiishara cha kuzikwa pamoja naye na kufufuliwa pamoja naye kinatimizwa kupitia tendo la ubatizo.
Galatia 3: 27.
Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo. (GAL. 3:27 SUV).
Tukibatizwa katika Kristo ni tendo ambalo linatupelekea kumvaa Kristo.
Kwa hiyo kimsingi tunaona kuwa ubatizo ni tendo la ishara la nje linaloonyesha kile ambacho kimefanyika ndani. Kwa hiyo kama tumekubali ya ndani tukubali na hili la nje pia.
Mungu akubariki sana.
Asomaye, afahamu.
 

Tuesday, November 18, 2014

NEEMA YA MUNGU..

 
Tito 2:11..

Neema ni upendeleo (Favour),au Katika tafsiri nyingine Neema ni usaidizi wa Kimungu (Divining Patronage).

Biblia inasema katika Tito 2:11 ( Maana Neema ya Mungu iletayo wokovu imefunuliwa), kufuatana na kitabu cha Tito "kwamba neema ya Mungu iletayo wokovu imefunuliwa, ikiwa na maana hakuna mtu anayeweza kuokoka au kumsogelea Mungu isipokuwa Neema ya ...Mungu imefunuliwa kwake. (Yohana 14:6)

Ukiangalia Yohana 14:6 inasema hakuna awezaye kwenda kwa Baba isipokuwa kupitia Mimi (Yaani Yesu Kristo),kwa lugha nyingine naweza kusema,ukifika mahali pa Kuokoka na kumpenda Yesu ujuwe ya kwamba si wewe,wala si nguvu zako ila ni Neema au usaidizi wa Mungu umekuvuta kwake.

Kwa lugha nyepesi vile ulivyo usijivune,usijigambe,usijiinue,ila Mshukuru Mungu kwa Neema Yake ya kuwa hivyo ulivyo,maana ni upendeleo juu ya Maisha yako.Jiulize umeshasafiri mara ngapi kwa umri uliokuwa nao?, Umeshaziona ajali ngapi kwa macho yako lakini huko salama Mshukuru Mungu maana ni neema yake imekufanya uwe mzima,kila kunapokucha Mshukuru Mungu kwa upendeleo wake.Sasa tuangalie 1Samweli 16:7-13.Utaona namna Mungu anavyojaribu kumfundisha mtumishi wake Samweli kwamba yeye(Mungu) aangalii uso,urefu wala kimo,na cha nyongeza wala elimu ya mtu.Kwa maana nyepesi Mungu avutwi kutuchagua tumtumikie kama watu wanavyochag...ua,yeye anaangalia moyo Pia ujue kwamba kuna kitu kinaitwa satanic grace(yaani neema au upendeleo wa shetani),utakuta mwanaume au kijana amezini na zaidi ya wanawake 50,na anajigamba kwamba atakama hana Hela wanawake wanamkubali tu,na upande wa pili kwa wanawake au wasichana,ujue huyu mtu amechaguliwa na shetani kujenga ufalme wa zinaa duniani,kwa hiyo nakuonya wewe mwenye roho hizo chafu,ujue unatumika kwa faida ya shetani na kwa hasara yako.
Utakuta familia ya watoto watano cha ajabu mikoba ya kichawi inamchagua mmoja,kwa nini? ni kwa sababu kibali cha kichawi kimemchagua mtu huyo,cha kufanya kataa kwa jina la Yesu mambo yote ya ki shetani atakama yanakupa sifa na heshima,shetani anakupenda na kukutumia kwa mapenzi yake then ataku damp(tupa)

BY: BISHOP DEO
(THE BODY OF CHRIST MINISTRY MOROGORO)
0717 660807

MAFANIKIO YAKO YA MWILINI NI MATOKEO YA MAFANIKIO YAKO YA ROHONI

3.YOHAN:1:2
 "Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo."

Shaloom mwana wa MUNGU, ninapenda kushare nawewe kwa ufupi sana somo hili ambalo MUNGU amenipa kwaajili yako.
 Labda wengi wetu tunaweza tukawa tumeshindwa kuelewa connection iliyopo kati ya yale tuyaonayo katika ulimwengu wa mwili na yale yaliyopo katika ulimwengu wa ROHO.
KWA KIFUPI YALE YANAYOTUKIA MWILINI nimuhimu ujue kwamba YALIANZIA ROHONI KWANZA. Hivyo uyaonayo mwilini ni matokeo ya ROHONI.
Na ndiyo maana ukisoma NENO LA MUNGU vizuri katika kitabu cha WAEFESO:6:12, Utaona kuna aina ya vita tunafundishwa namna ya kupigana, SASA MUNGU hataki tuangaike kupigana katika mwili kwa sababu ANAIONA HIYO VITA ULIYO NAYO SOURCE yake ni rohoni na ili TUSHINDE VITA nasisi inatupasa tuingie ROHONI.
Ndugu 3YOH:1:2 Unaiona sasa namna inavyo husianisha mafanikio yako katika kila jambo linalo husu maisha yako na KUFANKIWA KWAKO ROHONI.
Anasema NAOMBA UFANIKIWE KATIKA MAMBO YOTE KAMA ROHO yako ifanikiwavyo, KWAHIYO KAMA HAUJAFANIKIWA ROHONI NI VIGUMU KUFANIKIWA MWILINI, mafanikio ya rohoni HUDHIHILIKA MWILINI.
HIVYO KAMA UNATAKA MUME anza jambo kwanza rohoni, kama unataka kazi anza kwanza rohoni, kama unataka watoto anza kwanza rohoni, kama unataka kufanikiwa masomoni anza kwanza rohoni, FUTURE YAKO NAIONA IPO ROHONI anzia huko utauona ukuu wa BWANA.
UKIONA MTU KAENDA KWA MGANGA anataka afanikiwe kimaisha au apate kazi au awe na mvuto kwa wanaume aolewe JUA KWAMBA ANATENGENEZA ROHONI KWA KICHAWI, kwasababu waganga ni WACHAWI wa kawaida kabisa.
SIKIA MTU WA MUNGU hakuna msaada kwa waganga wa kienyeji KWANZA KABISA WENYEWE HAWANA HAYO MAFANIKIO UNAYO YAHITAJI watakulia fedha zako na kuku zako tu.
LAKINI LIPO TUMANI PALE MSALABANI tunakwenda kufanikiwa rohoni hadi mwilini katika kila jambo kwa jina la YESU
 OMBA NAMI SASA
 BWANA YESU ninakushukuru kwamaana UMENIPA ufahamu mpya juu ya UHUSIANO ULIOPO KATI MAFANIKIO YANGU ya rohoni na mwilini, SASA NIMEAMUA kuanza vita ya rohoni ili nipokee katika mwili, WALE WOTE walio funga mafanikio yangu katika ulimwengu wa roho kwa kichawi, MOTO wa BWANA UWATEKETEZE. KATIKA JINA LIWEZALO LA BWANA YESU KRISTO AMEEEEEEN... UBARIKIWE maana unakwenda kufanikiwa sasa.
N.BAMPELE-0762186639

Wednesday, November 5, 2014

KWA WAOAJI......

MWANANGU MPENDWA NAOMBA UNISIKILIZE KWA UZURI KABLA HUJAOA...

1.Mwanangu.
mwanamke anaweza kuwa mkeo,mwingine anaweza kuwa Mama watoto wako,lakini ukipata mwanamke ambaye atakuwa kama mama kwako,mama kwa wanao na mama kwa familia.tafadhari mwanangu usimuache huyo!

2.Mwanangu
Usimfanye mwanamke wako kuwa ndio wa kupika na kufanya kazi zote za jikoni peke yake,tabia hiyo siyo nzuri kwani hata ...nyakati zetu Mashamba yetu yalijulikana kwa majina yetu wanaume lakini tulifanya kazi pamoja

3.Mwanangu
Nikikwambia wewe ni kichwa cha familia,simaanishi kutuna kwa pochi lako,usiangalie kabisa pochi lako,angalia kama utaona tabasamu usoni kwa mke wako.Pesa sio kila kitu katika ndoa haileti ukuu wa familia!

4.Mwanangu
Ukitaka kuwa na maisha marefu na ukapunguza misongo ya mawazo,ongea na mkeo pangeni bajeti na mahitaji yenu,kasha mwache mkeo awe na jukumu la kuratibu mahitaji ya kila siku ya familia kwa kumkabidhi fungu husika hata kama limetokana na michango yenu wawili..
Wanawake wanajua sana kupanga bajeti na haitakuwa rahisi yeye kutumia hela hovyo,wakati akijuwa nyumbani kuna mahitaji ya msingi,lakini hela zikiwa kwako ataendelea kuomba hata kama utakuwa umeishiwa

5.Mwanangu
Usithubutu kumpiga mkeo,maumivu ya kipigo hukaa ndani ya moyo wake kwa muda mrefu sana na huacha kidonda ambacho hukawia sana kupona.Ni hatari sana kuishi na mwanamke mwenye majeraha moyoni

6.Mwanangu
Sasa unaamua kuoa,kama bado utaendelea kuishi maisha kama ya ubachela na mke wako,sio muda mrefu utakuwa bachela tena.Ukioa badilika anza kuishi maisha ya mke na mume.

7.Mwanangu
Zamani tulikuwa na wake wengi na watoto wengi kwa sababu tulikuwa na mashamba makubwa na mavuno yalikuwa makubwa,lakini kwa sasa maisha yamebadilika,kwa hiyo mkumbatie mwanamke wako peke yake kwani hakuna ardhi tena na mahitaji ya watoto ni makubwa sana.Angalia ukubwa wa familia yako!

8.Mwanangu
chini ya mwembe ambao nilikuwa nikikutana na Mama yako inaweza kuwa ni hoteli kubwa nyakati zetu,lakini kumbuka kitu pekee tulichoweza kufanya chini ya mwembe ilikuwa ni kukumbatiana pekee,Nakushauri ukikutana na marafiki wa kike kikubwa unachoweza kufanya nao ni kupeana mikono na ikizidi ni kukumbatiana hadharani na si vinginevyo.

9.Mwanangu
Usibadilike mara utakapoanza kupata mafanikio zaidi kuliko kuwahudumia hao viruka njia wa mtaani ambao hawajui mmetoka wapi na mkeo nakushauri utumie na kufurahia mafanikio yako na mkeo ambaye aliweza kusimama imara wakati wote wa mapito yenu magumu

10.Mwanangu
Kumbuka unapoanza kusema au kuona mke wako kabadilika,ujue kuwa kuna kitu ambacho ulikuwa unakifanya umekiacha kukifanya.Jitathmini na anza kufanya au kutimiza wajibu wako

11.Mwanangu
Usijaribu kumfananisha au kumlinganisha mke wako na mwanamke mwingine wa nje,kwani hata yeye anakuvumilia sana na hajakufananisha na mwanaume mwingine yoyote huko nje na ndio maana aliamua kuwa na wewe.

12.Mwanangu
Sasa hivi kuna hiki kinaitwa haki za wanawake,ni sawa kama mwanamke anasema ana haki sawa na wewe katika nyumba basi gawanya mahitaji yote ndani kwenu katika sehemu mbili zilizo sawa,halafu timiza nusu yako na mwambie atimize nusu iliyobaki

13.Mwanangu
Nilimuoa Mama yako akiwa bado kigoli (Bikra) na nilikuwa naenda sana kwao kabla sijamuoa,lakini kutomkuta mkeo bikra kusikufanye umalaumu kuwa alikuwa muhuni kumbuka,wanawake wa Enzi zetu na wasasa ni tofauti,ulimchagua mwenyewe, na ukigoli hukuujua kabisa.Usiingize mambo ya kabla ya ndoa kwenye ndoa yenu.

14.Mwanangu
Sikuwapeleka Dada zako shule kwa kuwa nilikuwa njinga kama wazee wengi wa hapa kijijini wasemavyo,tafadhari usifanye ujinga huu,kwani kiwango cha mafanikio ya wanawake wa sasa kimefanya wanaume waonekane ni watu wa kawaida sana na sio muhimu kama Enzi zetu.Ukijaliwa watoto wape elimu.

15.Mwanangu
Zamani Enzi za ujana wetu,wanawake walikuwa na urembo wa asili,ingawa siwezi kukudanganya,wengine waliongeza urembo kwa kujichora hina na hata kutoboa pua na masikio lakini usisahau hawakuonesha maumbile yao na nyeti hadharani

16.Mwanangu
Mama yako na mimi hatuna hisa katika kila kitu kinachoendelea katika maisha yenu,Jaribuni kutatua changamoto zenu wenyewe bila kila mara kuja kwetu kuomba usuluhishi.Ndoa ni pamoja na ukomavu wa kutatua changamoto zenu bila kuziuza kama gazetini kwa kila mtu.

17.Mwanangu..
Nilimnunulia mama yako kifaa cha kupikia vitumbua ili aanzishe mradi wa kuuza vitumbua,pia nilimsaidia kununua cherehani yake ya kwanza,Tafadhari msaidie mke wako kutimiza ndoto zake kulingana na uwezo wako kama ambavyo unahangaika kutimiza ndoto zako

18.Mwanangu usiache kutusaidia mimi na mama yako,utu uzima una changamoto nyingi sana na Mungu akikujalia utaziona muda ukifika.Pamoja na kutimiza majukumu yako kama Baba wa familia kumbuka pia bado tunaishi na wewe ni motto wetu.

19.Mwanangu...
Kila upatapo muda wa kuomba,omba na familia yako,kuna kesho ambayo huijui,ongea na MUNGU wako ambae anajua kila kitu kila siku

20.NAKUTAKIA MAISHA MEMA YA NDOA MWANANGU NAKUPENDA

KWA VIJANA.......

Biblia inasema, "Kumcha Mungu ni kuepuka(kukwepa) uovu" na pia inasema, "Zikimbieni tamaa za ujana" lakini pia inasema, "Ikimbieni zinaa" ....Lakini cha ajabu ni kwamba vijana wengi wanafanya kinyume na Biblia inavyosema, hawakai mbali na mazingira hatarishi yanayoweza kuwapelekea kufanya mambo ya ajabu....Utakuta kijana anaishi room na ma room-mate wanaongea vumbi(pumba) halafu naye anakaa tu...anajisemea moyoni mwake, "Nitasikiliza tu ila sitafanya kama wao" ...Usiwe mpumbavu, Mungu anajua udhaifu ulionao katika mwili wako,ndo maana anasema, "Heri mtu yule...asiyeketi barazani pa wenye mizaha" ...Maneno wanayoyasema yatapanda mbegu fulani,ambayo mwisho wa siku itakomaa na itatoa matunda ambayo hautayapenda...Utakuta mkaka/mdada anaongea na simu (hasa usiku-mida ya xtreme au boom club nk) mpaka simu inakuwa ya moto,inaishiwa chaji,anaichaji na ana 'keep talkin' tangu saa 5 usiku hadi 8usiku,..Muda wote huo anaongea na mtu mmoja...tena wa gender ingine...mnaongea nini 3 consecutive hours?...Najua siku ya hukumu kuna watu wataona hata aibu kusikia maongezi yao...wengine watatoa macho watakapoambiwa wasome sms zao na wengine wataduwaa wakiletewa chat-mail zao...kuna mambo mengi sana mnayoyafanya nyuma ya pazia...mkiwa peke yenu huku Mungu akiwatazama...Self discipline ni ya muhimu sana, we mkaka utakaaje na mdada kwenye 'angle mbaya' mpige story masaa kadhaa...unajua nia ya huo mwili wako? NIA ya Mwili ni Uadui dhidi ya Mungu(Warumi 8:6-7) ...Utakuja kushtuka tayari umefanya vituko...jitahidi ufanye kile Biblia inachosema: Epuka uovu... Zikimbie tamaa za ujana...Ikimbie zinaa...Haisemi OMBA au Funga siku kadhaa!

MTEGO WA MWINDAJI

Zaburi:91:3’’Maana yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji,..’’
Namshukuru MUNGU aliye nipa kibari cha kushiriki na wewe somo hili la MTEGO WA MWINDAJI, ambalo naamini linakwenda kukusogeza hatua nyingine kabisa katika imani yako.
KIKAWAIDA MTU UNAPO SEMA KWAMBA umeokoka yani umejiunga na uzao mteule wa mwanakondoo, MOJA KWA MOJA huwa unakuwa umetangaza uadui na UFALME WA GIZA.

Hiv...yo acha nikuite kuwa wewe ni mwana vita au mpiganaji au mpambanaji(ni mwanajeshi wa jeshi la mwana kondoo). WAEFESO:6:12 ‘’Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu na roho’’. HAPO UNAWEZA GUNDUA KITU KUMBE WEWE NI MTU wa mashindano LAKINI hayo mashindano hayapo juu ya DAMU na NYAMA, yapo katika ULIMWENGU wa roho, HIVYO kama mkristo ni muhimu uwe na uwelewa wa ULIMWENGU wa roho ili uweze KUPAPAMBANA vilivyo la sivyo UNAWEZA UKAPIGWA NA ADUI.

Sasa twende kwenye somo letu rasmi, MTEGO WA MWINDAJI: Hapa kwanza kabisa na mzungumzia MWINDAJI pamoja na mtego alio utega kwaajili ya anacho kiwinda(anaye windwa). Lakini pia tumwangalie na MWOKOZI(Anaye okoa) wa hii mitego iliyo tegwa na mwindaji.
Katika kufuatilia kwangu nimegundua ya kwamba TUNA WAKRISTO wengi makanisani wanaohudhulia ibada vizuri sana, na niwatoaji wazuri sana wa mafungu ya kumi, LAKINI WAKRISTO wengi wana fikiliaga kwamba kuitwa mkristo peke yake inatosha, WANASAHAU yakuwa adui(SHETANI) Huwa bado anaandaa mitego ya kuwatoa kwenye imani walizo nazo, 1PETRO:5:8 ‘’ Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.’’

Unaona sasa kumbe bado kuna mtu anatafutwa ili amezwe, sasa hapa unaona kutokana na mawindo ya SHETANI anafananishwa na SIMBA aungurumaye akitafuta mtu ammeze, hivyo yupo mawindoni, yeye hali swala, nyati wala punda milia, ndiyo utofauti ulipo hapa wa huyu mfano wa simba, yani yeye chakula chake ni watu tu. So anaweza akakumeza wewe au mimi TAKE CARE.
TUNA MZUNGUMZIA SHETANI kama mwindaji sasa, ambaye ametega mitego yakutosha kwa ajili yako, ili akurudishe nyuma kiimani, aivunje ndoa yako, akurudishe nyuma kiuchumi n.k

Labda acha nikupe kitu kidogo kinacho weza kukusaidia juu ya mwindaji. SHETANI mawindo yake hayakuanza leo, alianza tangu pale EDENI, alimuwinda ADAM kwa muda mrefu ili amtoe kwenye kusudi la MUNGU, na kuuharibu uhusiano uliopo kati ya ADAMU na MUNGU. Aliubadilisha UKWELI kuwa UONGO ili tu ADAMU aingie mtegoni, na kweli alifanikiwa katika hilo. Soma MWANZO:3

NOTE:SI KILA JAMBO LIJALO KAMA BARAKA, NI LAKULIKUMBATIA NA KULIONA LA FAA SANA; MAMBO MENGINE YAMEKUJA KAMA BARAKA KWETU LAKINI NI MTEGO HALISI WA MWINDAJI.
Nimeona watu wengi kutokana na hali ambazo wamekuwa wakizipitia katika maisha yao wamejikuta wakinaswa na mtego wa mwindaji, wengine ni kweli walisimama kiimani lakini walisahau ya kuwa bado walikuwa wanawindwa na mwisho wake ukawa nikuangukia katika mtego wa mwindaji.
NIOMBI LANGU KWA MUNGU AKAITEGUE MITEGO YOTE ILIYO TEGWA DHIDI YA KILA ENEO LINALO HUSU MAISHA YAKO KATIKA JINA LA YESU KRISTO ALIYE HAI.

Naomba nikukumbushe kitu mwana wa MUNGU, shetani hajakutega katika hii leo yako unayoiona ni ya baraka kwako au ni ya furaha kwako, LAKINI NAUONA mtego alioutega kwa ajili yako ni KWAAJILI YA KESHO yako, maana amekutazama akagundua kwamba wewe ni mtu watofauti sana, na mwenye impact(matokeo) kubwa sana kwa wakati ujao wa maisha yako, KWAHIYO NI MUHIMU KUJUA KWAMBA taabu unayoipata leo ni matiokeo ya mtego uliowahi kutegwa na ukategeka kwa wakati huo ulio pita.

HEBU tusogee mbele zaidi sasa. 1Samweli:18:21 ‘’ Naye Sauli akasema moyoni, Mimi nitamwoza huyu, awe mtego kwake, tena mkono wa wafilisti uwe juu yake.’’
Hapa sasa unaweza kuona sasa kumbe kunawatu wana ndoa zilizo mitego kwao, Hapa utamwona SAULI anamwozesha binti yake kwa DAUDI si kwamba awe mke bali awe mtego kwa kwa DAUDI. Anhaa.. Kumbe MUWINDAJI anaweza akakuletea mume/mke ambaye ulikuwa ukimwomba MUNGU kwa muda mrefu, nawewe ukajipa moyo kwamba tayali MUNGU amejibu maombi yako, kuumbee ni MUWINDAJI amekuletea mfano wa mume/mke ili apate kukuingiza au kukunasa mtegoni, HATAKAMA UTASUBIRI KWA MUDA GANI JUA KWAMBA MUNGU NDIYE ATAKAYE KUPA MWENZA WAKO, JIANGALIE USIJE ANGUKIA MIKONONI MWA WANYANG’ANYI..



Thursday, March 27, 2014

Sikia Mtu wa MUNGU

SIKU HIZI KUNA WIMBI LA SMS ZENYE NUKUU YA MISTARI YA BIBLIA AU MCHORO WA MSALABA,

SMS HIZI HUKUTAKA MTU UTUME KWA IDADI KAZAA YA WATU NA UNAAHIDIWA BARAKA KWA KUTEKELEZA NA LAANA KWA KUPUUZA.

Ukweli ni huu,
1.kuna aina 42 ya misalaba ambayo ni alama za freemason ukiwemo unaosambazwa ktk sms

2.Watu hulaaniwa kwa kutotii amri za Mungu na si kutotuma sms

3.Huwezi kumpangia Mungu kubariki n...dani ya siku fulani,

4.Hakuna mahali ktk biblia ambapo Yesu alilazimisha watu wamhubiri akiwatishia laana na kuwahonga baraka.

5.Daima sauti ya Yesu ni ya upole,

6.kuwa makini usìje ukamtumikia shetani.

NA MUNGU WA MBINGUNI AKUBARIKI
 
 

Saturday, February 8, 2014

Jehanum ya Moto ni Wapi na Kukoje?

Miaka kadhaa iliyopita, nilikuwa nimezama sana katika dhambi. Nilipokuwa katika lindi hilo la dhambi, sikutaka kusikia chochote kwa mtu yeyote aliyenieleza kwamba niache dhambi, na eti niokoke. Niliwaona watu wanaohubiri mambo ya kuokoka, wameshindwa maisha, wamechanganyikiwa (frustrated), na tena

hawajasoma . Nakumbuka siku moja, mhubiri mmoja alinihubiri na kuniambia, ”Acha dhambi, au sivyo utatupwa katika Jehanum ya moto.“ Unajua nilimjibuje! Nilimwambia, ”Wewe usinibabaishe na hiyo Jehanum ya moto. Potelea mbali nikienda motoni, pilipili usizozila zakuwashia nini? Usinifuatefuate katika maisha yangu, chukua ”time“ yako!

Baada ya miaka kadhaa kupita, nilipokuja kusikia mafundisho kuhusu jinsi kulivyo huko Jehanum ya moto, nilikuja kufahamu kwamba yule mhubiri nilimjibu ”potelea mbali nikienda motoni“, kwa sababu tu sikuwa ninaelewa lolote kuhusu jinsi Jehanum kulivyo; kwa kuwa sikuwahi kufundishwa mafundisho hayo na kiongozi

wangu wa dini. Tangu niliposikia mafundisho hayo, maisha yangu yalibadilika kabisa. Mpendwa msomaji, huenda hata wewe hujasikia mafundisho halisi kuhusu jinsi kulivyo Jehanum ya moto, kama mimi nilivyokuwa; ndiyo maana nimeona leo nikushirikishe mafundisho haya kupitia katika tovuti hii. Mungu akubariki kwa kuendelea kusoma ujumbe huu.

Biblia inaeleza waziwazi kwamba mtu anapokufa, sekunde ileile ya kufa kwake anakabiliwa na hukumu. Tunasoma katika WAEBRANIA 9:27, ”Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu.“ Watu wanaofundisha kinyume na kweli ya Neno la Mungu, hufundisha kwamba mtu anapokufa, analala

tu, na hakuna lolote la hukumu mara moja wakitumia maandiko yafuatayo na kuyatafsiri visivyo: MATHAYO 27:52; 1WAKORINTHO 15:20: YOHANA 11:11-14 n.k.; na pia wanasema wafu hawajui lolote kwa kutumia maandiko kama MHUBIRI 9:5. Ilivyo ni kwamba, kinachobaki kaburini ni mwili tu. Roho ya mtu huondoka na kuingia katika mwili mwingine, unaoitwa mwili wa roho Miili tuliyo nayo wanadamu kabla ya kufa, inaitwa miili ya asili. Tunasoma katika 1WAKORINTHO 15:40, 44, ”Tena kuna miili ya mbinguni, na miili ya duniani, …Ikiwa uko mwili wa asili, na wa r oho pia uko.“

Mwili wa asili, ndio unabaki kaburini, lakini roho ya mtu huondoka kama tunavyosoma katika MHUBIRI 12:7, Nayo mavumbi ya nchi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.“Mwili wa asili, ndio unaobaki kaburini, na huo ndio unaotajwa kwamba umelala, haujui lolote, na hauna kumbukumbu; lakini pasipo mwili huo, mtu atamwona Mungu na kukabiliana na hukumu yake dakika ileile baada

ya kufa (AYUBU 19:26). Ikiwa mtu ameishi katika mapenzi ya Mungu, mara tu baada ya kufa huchukuliwa mbinguni (LUKA 23:43; 16:22). Ikiwa ameishi na kufa katika dhambi, bila kutubu dhambi zake na kuokoka, hukumu yake mtu huyo, huwa ni kutupwa katika Jehanamu ya moto, mara tu baada ya kufa, kama yule tajiri anayetajwa katika Biblia (LUKA 16:19-24).

Mbinguni ni juu (Mbingu ya tatu), lakini kuzimu au Jehanamu ya moto, ni pande za chini zanchi (2 WAKORINTHO 12:1-4; MITHALI 15:1-4; MITHALI 15:24; ZABURI 63:9; EZEKIELI 31:14. Mara mtu anapokufa, hufika kwenye njia panda. Kila mmoja hupenda kwenda mbinguni kuzuri, hata hivyo ikiwa jina lake haliko katika kitabu

cha uzima cha mbinguni, hulazimika kwenda Jehanum ya moto. Mtu anayetakiwa kwenda motoni, huchachamaa na kukataa kwenda kwenye njia mbaya inayotisha ya motoni. Hali hii wakati mwingine inaweza kuonekana katika mwili wa asili kwa kumwangalia mtu anavyotapatapa na kuhangaika sana katika kufa kwake. Kutokana na mtu asivyopenda kwenda motoni na kutaka kwenda mbinguni asikotakiwa, mtu hulazimika kukamatwa kwa nguvu na malaika wa kutisha, na kutupwa katika Jehanum ya moto; inayojulikana pia kwa jina jingine, giza la nje; kama

tutakavyoona baadaye kidogo (UFUNUO 19:20; 20;10; MATHAYO 25:30).

Huko motoni Jehanum kukoje? Kunatisha, nashindwa hata nikueleze vipi unielewe. Moto wa milele, hatukuwekewa wanadamu bali shetani na malaika zake (MATHAYO 25:41). Kama utakwenda huko baada ya kusoma ujumbe huu, itakuwa ni kwa sababu ya kiburi chako tu, na kushupaza shingo yako na kukataa kulitendea kazi Neno hili (MITHALI 29:1). Moto wa Jehanum siyo mahali pa mchezo kama walimu wa uongo wanavyofundisha. Waalimu hawa huwafariji watu na kusema eti mtu ataunguzwa na moto na kutoweshwa na kuangamizwa kabisa na ndiyo mwisho wake. Wanatumia maandiko kama MATHAYO 10:28 (kuangamizwa) na YOHANA 3:16 (kupotea). Kuangamia katika maandiko hayo haimaanishi kumalizika kabisa, bali kukabiliwa na mauti (ESTA 4:16). Mauti ya watu walioko motoni, ni mauti ya milele, kama tutakavyoona hivi punde. Kondoo akipotea, haimaanishi hayupo kabisa ila ametengwa na mchungaji (ISAYA 57:1-3).

Vilevile, neno ”Kuharibu“ linapotumika kuhusiana na adhabu ya milele, halina maana ya kufanya kitu kisiwepo, bali ni kuadhibu vikali (1WAKORINTHO 3:16-17. Waalimu hawa wa uongo, pia hufundisha pia kwamba, eti watu watatoweshwa kama moshi baada ya kuunguzwa kwa kutumia andiko la ZABURI 37:20. Kutoweshwa hapa ni

kutenganishwa na Mungu, kama Adamu na Hawa walivyotoweshwa na kutolewa katika bustani ya Edeni, na hivyo kutengwa na Mungu, Kwa ujumla, mafundisho yote haya yanayotokana na Shetani, yanalenga kuwafanya watu waendelee kutenda dhambi, huku wakipuuza ukweli juu ya Jehanum, kwa kuwaza kwamba watateseka dakika chache na kupotea kabisa na ndiyo mwisho. Hiyo siyo kweli.

Ukweli kuhusu Jehanum ya moto ni upi basi? Sikiliza nikuambie! Jehanum ya moto, au Kuzimu, ni shimo kubwa na refu sana lililojaa moto. Wengi tunafahamu jinsi wanawake wanavyouchochea moto wa kuni au mkaa, kwa kuupulizia hewa kwa mdomo, au kipepeo. Sasa basi, moto wa Jehanum nao huchochewa mfululizo, ili usizimike; lakini huchochewa na pumzi ya Bwana, yaani pumzi maalum ya Mungu mwenyewe (ISAYA 14:15; 30:33). Moto wa Jehanum ni mkali sana kuliko moto wowote tunaoufahamu duniani. Moto wa gesi wa kuunganishia vyuma, unaotokana na kuwashwa mchanganyiko wa gesi ya ”Oxygen“ na ”Acetylene“, moto huu unaonekana kwa hapa duniani kwamba ni mkali. Moto huu, siyo chochote, ukilinganishwa na moto wa Jehanum. Katika karakana au viwanda vinavyotengeneza vifaa vya chuma, chuma huyeyushwa na kuwa ujiuji katika matanuru ya moto mkali unaofikia nyuzi joto 2,000 hadi 3,000 na zaidi. Moto huu unaoyeyusha vyuma na ukali wake, huo si chochote! (Kumbuka kwamba maji yaliyochemka sana hufikia nyuzi joto 100 tu!). Moto ulio katikati ya jua linalotuangaza, unafikia nyuzi joto milioni kumi . Moto wa jua nao, si chochote ukilinganishwa na moto wa Jehanum! Ukali wa moto wa Jehanum, unatisha (WAEBRANIA 10:26-27). Siyo hilo tu, moto wa duniani una rangi mbalimbali, njano, bluu, nyekundu n.k. Moto wa Jehanumu ni tofauti kabisa; Ni moto wa rangi nyeusi, unaosababisha giza na kumfanya mtu aliye motoni, awaone wenzake wachache tu wa karibu naye, hivyo hamna faraja ya kusema ”tuko wengi!“ Moto huu mweusi, ndiyo maana unaitwa ”giza la nje“ Mathayo 8:11-12, 22:13; 25:30; YUDA 1:6). Siyo hilo tu. Moto huu wa Jehanum, una meno! Hivyo una uwezo wa kuwala na kuwatafuna walioko motoni (KUMBUKUMBU 32:22; WAEBRANIA 10:26-27). Hata hivyo, pamoja na moto huu kumtafuna mtu, bado una sifa ya kumhifadhi mtu huyo na kumfanya asimalizike, kama jinsi chumvi ilivyo na uwezo wa kuizuia nyama kuharibika. Hivyo moto unamtafuna mtu wakati wote, lakini haishi na wala moto wenyewe hauzimiki. Ndiyo maana unaitwa moto wa milele (MARKO 9:43-49; MATHAYO 25:41).

Moto huu wa Jehanum, huambatana na madini yanayoitwa kiberiti au kwa lugha ya kitaaluma, Sulphur.“ Kwa wale wanaofahamu kidogo somo la shule la ”Kemia,“ au ”Chemistry,“ wanafahamu kwamba madini ya ”sulphur“ yakiwashwa moto, huwa kama mpira, na hutoa harufu mbaya kama ya mayai yaliyooza. Harufu ya namna hii

inafunika kuzimu yote, na watu walioko huko wanahangaika kushika pua zao, lakini hakuna jinsi! Hebu jaribu kuwaza maisha haya, ndiyo yawe ya milele, mpendwa msomaji! Siyo hilo tu! Katika moto huu, wamo funza maalum ambao huwatafuna watu na kufanya matundu mengi makubwa katika miili yao, wakiingia na kutoka, kutoka ubavu hadi ubavu mwingine, kutoka kwenye tumbo hadi mgongoni n.k. Hii hufanya sura za wale walioko motoni, kuwa mbaya mno kama madude tu! (ISAYA 14:11; MARKO 9:43-49; ISAYA 66:24). Hata kama mtu alikuwa mweupe duniani, huko motoni, huwa ni mweusi tii!

Moto wa milele, huitwa pia mauti ya pili (UFUNUO 21:8). Kwa nini huitwa mauti ya pili? Uchungu wa mauti unaomfanya mtu kugugumia kwa mateso makali, akishindwa kupumua vizuri na kubaki kusema ”Mmh! Mmh! Mmh!, mpaka watu wanasema heri afe apumzike, uchungu wa jinsi hiyo humkabili mtu aliye motoni, milele na

milele. Kwa lugha rahisi, ni kusema kwamba watu walioko motoni, wakati wote wako katika hali ya kufa, lakini hawafi! Niseme nini ili unielewe! Watu walioko motoni, hujawa wakati wote na vilio, na tena husaga meno yao kama mtu anayeona baridi kali (MATHAYO 8:12). Walioko motoni wanajifahamu, na kuwakumbuka wenzao waliowaacha duniani, na tena wakati mwingi hutoa ndimi zao nje, kama mbwa, wakitamani maji kidogo kupoza ulimi kutokana na joto kali linalosababisha kiu kubwa, lakini hawapati maji hata tone! Juu ya yote hayo katika vilio vyao, humwomba Mungu awahurumie na kuwasamehe lakini Yeye amekwishasema, Nami jicho langu

halitaachilia, wala sitaona huruma (EZEKIELI 9:10; 8:18).

Watu walioko motoni, hutamani mtu mmoja kati yao atoke motoni aje duniani, awashuhudie ndugu zao, ili waache dhambi, na kukwepa mateso yao, lakini huambiwa kwamba ndugu zao wanapaswa kuyasikia maneno ya manabii walioko duniani, maana hata akitumwa mtu kutoka motoni na kuelezea mateso ya huko, watasema ni mwongo, hajaenda motoni. Tunasoma haya katika LUKA 16:27-31, ”Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu, kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali

hapa pa mateso. Ibrahimu akasema, wanao Musa na manabii, wawasikilize wao. Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea watu atokaye kwa wafu, watatubu. Akawaambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa (hawatashawishika) hata mtu akifufuka katika wafu.“

Mpendwa msomaji, ikiwa mama yako mzazi alifariki akiwa hajaokoka, ujue yuko motoni, na anakuambia, ”Usinifuate huku mwanangu“. Ikiwa baba yako mzazi alifariki akiwa dhambini, anateseka motoni, na hataki umfuate huko aliko! Ndugu, marafiki na jamaa zako walioko huko wanakukumbuka sana, na hawapendi ujiunge nao huko,

bali wanataka utubu na kuokoka mateso hayo ya moto. Walioko huko motoni, wakimwona yeyote mwingine kutoka duniani, ambaye alikuwa na nafasi ya kusikia habari kama hizi na akazipuuza, kisha akawafuata huko motoni, humwambia, ”Je, wewe nawe umekuwa dhaifu kama sisi! Wewe nawe umekuwa kama sisi!“(ISAYA 14:10).

Mpendwa msomaji, baada ya kusikia yote haya kutoka kwa nabii aliyetumwa kukuletea ujumbe huu, usifanye moyo wako kuwa mgumu. Hii ni nafasi ya kipekee ya kuokoka. Je, unajuaje kama utaamka kitandani baada ya kulala usiku wa leo? Wakati uliokubalika wa wokovu ni sasa (2WAKORINTHO 6:2). Labda unajiuliza, ili uokoke, ufanyeje? Jibu ni rahisi. Kwa imani ukitubu dhambi zako huku ukimaanisha kuziacha, na kumwambia Yesu Kristo akusamehe, utasamehewa sasa hivi, na msamaha wa dhambi, huambatana na wokovu (LUKA 1:77). Je, uko tayari kuokoka sasa hivi? Najua uko tayari.Basi fuatisha sala hii kwa dhati toka moyoni,



”Mungu Baba asante kwa kuniletea ujumbe huu. Natubu dhambi zangu zote, kwa kumaanisha kuziacha. Yesu Kristo nakuomba unisamehe dhambi na kuniokoa kutoka katika mateso ya moto wa milele. Asante, kwa kuniokoa, katika Jina la Yesu. Amen. Tayari sasa umeokoka, na kwa hakika utakwenda mbinguni, hata ukifa leo. Ili uzidi kuukulia wokovu, hakikisha unahudhuria mafundisho katika Kanisa linalohubiri wokovu. MUNGU AKUBARIKI !!!

Friday, February 7, 2014

SABABU SABA ZA KIBIBLIA KWA NINI WATU WANAKUFA MAPEMA


Bwana Yesu asifiwe sana wana wa Mungu, ni matumaini yangu na Imani yangu ya kwamba u mzima na ya kuwa unaendelea kuufurahia uzuri wa Yesu Kristo na kazi yake ya msalaba.
 Leo ninataka kwa pamoja tuyachunguze maandiko na tuzipitie sababu hizi saba za Kibiblia ni kwa nini watu wengi wanakufa mapema...na sasa ongezeko la vifo vya mapema ni kubwa kuliko hata zamani. Kwa Tanzania wastani wa kiwango cha maisha ni miaka 45,Binafsi nauona umri huu kuwa ni mdogo sana kwa mtu wa rika hili kuondoka duniani kwani anakuwa na majukumu mengi ya kufanya na pia mchango wake unakuwa unahitajika kwenye familia, ukoo, wilaya, mkoa, taifa na hata duniani kwa ujumla.
 Ni maombi yangu na dua yangu kwa Bwana ya kwamba umalizapo kusoma ujumbe huu, macho yako ya ndani yatafunguka na utaweza kuona swala hili kwa jicho la Rohoni...KARIBU SANA.
                Zifuatazo ni sababu saba kwa mujibu wa Neno la Mungu ni kwanini watu wanakufa mapema(katika umri mdogo)
 1.KUTOWAHESHIMU WAZAZI(BABA NA MAMA)
 Biblia iko wazi sana na imesisitiza uhusiano mzuri na wa uhakika kati yetu na wazazi wetu...kinyume chake LAANA zitayaandama maisha yetu na maisha yetu hayatakuwa ya heri na marefu.
 Ukisoma Waefeso 6:1-3 inasema, "Enyi watoto watiini WAZAZI wenu katika BWANA, maana hii ndiyo HAKI.Waheshimu baba na mama yako, amri hii ndiyo ya kwanza YENYE AHADI (za ustawi, baraka na wingi wa miaka), upate HERI, UKAE SIKU NYINGI( UISHI SIKU NYINGI) katika dunia"   pia katika Kumbukumbu la Torati 5:16 Biblia inasema, "Waheshimu BABA na MAMA yako; kama BWANA, Mungu wako alivyoamuru, SIKU ZAKO ZIPATE KUZIDI, nawe upate KUFANIKIWA katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako"
 Kwa mujibu wa maneno ya Mungu hapo juu ni dhahiri kabisa ya kuwa watu wote wasiowaheshimu wazazi wao, ni ngumu kufanikiwa, Laana zinawafuatilia na zaidi ya yote wana muda mchache wa kuishi...WANAKUFA MAPEMA!
 2.KUKOSA MAONO
  Kwa mujibu wa Biblia, mtu anayeishi ili mradi tu, asiyejua kwanini yupo duniani, asiyekuwa na kusudi na mpango katika maisha yake, na asiyeweza kupanga hata mipango ya 'kesho nitafanya a, b, c nk' yuko katika hatari kubwa ya kuondoka duniani kabla ya muda wake...Biblia inasema, "Pasipo MAONO watu huangamia"....Biblia ya kiingereza inasema, "Without VISION people PERISH"
 Jitahidi kuwa na maono ya muda mfupi na ya muda mrefu, Mungu anashughulika na walio nacho, wasiokuwa nacho hata kile kidogo walichonacho hunyang'anywa.
 3.KUTOKUMCHA MUNGU
 Kumcha Mungu ni kuishi maisha yanayoongozwa na HOFU ya MUNGU (si woga dhidi ya Mungu)...Ni maisha ambayo moyo,mwili, nafsi na roho ya mtu inakuwa imejawa na kiu na njaa ya kumpendeza Mungu na kuyafanya maagizo yake yote-tena kwa furaha.
 Mithali 10:27 inasema, "KUMCHA BWANA kwaongeza siku za mtu, Bali miaka yao WASIO HAKI itapunguzwa"  na pia Mhubiri 7:17 inasema, "Usiwe MWOVU kupita kiasi; wala usiwe mpumbavu; kwanini UFE KABLA YA WAKATI WAKO?"
 Kwa mujibu wa ushahidi huu wa Neno la Mungu, ni dhahiri kuwa maisha yasiyo na uchaji na yasiyoongozwa na hofu ya Mungu, yanawafanya wengi wafe kabla ya muda wao waliokusudiwa kuishi.
 4.KUMWEKEA MUNGU MIPAKA
 Hii ni hali ya mwanadamu kuamini kuwa Mungu anaweza hili na hili hawezi...kitendo hiki Mungu anakiita kuwa ni 'DHARAU' kwake... Zaburi 78:41 inasema, "Wakarudi nyuma wakamjaribu MUNGU; Wakamwekea MPAKA Mtakatifu wa Israel"
 Mstari huu wa Zaburi unaelezea maisha ya wana wa Israel njiani toka Misri kwenda nchi ya Maziwa na Asali-Kanaani.
 Biblia inaeleza jinsi Musa alivyowatuma wapelelezi 12 kwenda kuipeleleza nchi ya ahadi waone kama kama kweli ni nchi ya 'Maziwa na Asali'...10 kati yao Waliporudi walirudisha ripoti ya kuwa kweli ile nchi ni ya maziwa na asali, ila inakaliwa na Wanefili-wana wa Anaki...majitu na ya kwamba wao ni kama panzi tu na hawawezi kwenda na kuimiliki. Joshua na Kalebu walileta habari njema...waliona kwa macho lakini wakazungumza kile ambacho ni 'UHAKIKA WA MAMBO YATARAJIWAYO' wakamwamini Mungu kuwa aweza kuwapa ile nchi kuwa milki yao sawa na alivyomwapia Ibrahim(Hesabu sura ya 13 na ya 14) na wote waliomwekea Mungu mpaka walikufa huko jangwani, hawakuingia nchi ya ahadi...WALIFUPISHA MAISHA YAO KWA KUTOKUAMINI KWAO...Ila Kalebu aliishi muda mrefu sana, alikuwa na nguvu kama za mtu wa miaka 40 hata alipokuwa na miaka 85( soma Joshua 14:6-14) na inaeleza pia ya kuwa Joshua alikuwa MZEE SANA, alikufa akiwa na miaka 110 lakini alikuwa na nguvu zake kamili mpaka pale BWANA alipompumzisha(Joshua24:1-29)
 Kama unataka kuwa na maisha marefu, na unataka kuziongeza siku zako...ishi maisha ya IMANI...Usimwekee Mungu mipaka, kumbuka, "Njia zake zi juu mno na fahamu zake pia" Isaya 55:8-11
 5.KUTOKUMTUMIKIA MUNGU
 Biblia inasema katika KUTOKA 23:25-26, " Nanyi  mtamtumikia BWANA, Mungu wenu naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; NAMI nitakuondolea Ugonjwa kati yako...na  hesabu ya SIKU zako nitaitimiza"
 Huu ni ukweli ambao inabidi uufahamu na uweke kwenye matendo.Unataka kuishi muda mrefu hapa duniani? kazi ni rahisi...fanya sehemu yako, MTUMIKIE BWANA naye ATAITIMIZA hesabu ya siku zako...HAUTAKUFA KABLA YA WAKATI.
 6.MAISHA YA DHAMBI
 Dhambi ni mbaya...inakutenga mbali na Mungu( Isaya 59:1-2) lakini kibaya zaidi inapunguza maisha yako...inakufanya ufe kabla ya muda wako...Unafurahia kuishi maisha ya dhambi? ni mzinzi, mwongo, msengenyaji, usiyesamehe,mwenye kinyongo, kisasi nk? Unajipeleka kaburini kabla ya wakati wako...unafanya kazi ambayo mshahara uitwao 'MAUTI' utaupata.
 Katika Warumi 6:23 Biblia inasema, "Kwa maana mshahara wa DHAMBI ni MAUTI(KIFO), bali karama ya Mungu ni uzima wa Milele katika Kristo Yesu Bwana wetu"  pia Biblia inasema, "Roho itendayo DHAMBI ndiyo itakayokufa"
 Maisha ya dhambi yanakata muda wa mtu wa kuishi...Ni wangapi waliokufa wakiwa vijana wadogo kwa sababu ya UKIMWI kwa kutoikwepa dhambi ya Uzinzi? au ni Wezi wangapi wamekufa wakiwa katika harakati za kuiba?
 Dhambi ni adui mkubwa kwangu na kwako!
 7.KUKOSA BIDII KATIKA KUMPENDA MUNGU
 Biblia iko wazi katika Zaburi ya 91:14-16, nayo inasema, "Kwakuwa AMEKAZA(Ameweka bidii katika) KUNIPENDA, Nitamwokoa; na kumweka palipo juu (NITAMWINUA) kwa kuwa amenijua Jina langu. Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni. Nitamwokoa na kumtukuza; KWA SIKU NYINGI nitamshibisha, Nami nitamwonyesha wokovu wangu"
 Biblia inasema Atakayekaza/kuwa na bidii katika KUMPENDA MUNGU atashibishwa kwa WINGI WA SIKU.
 Yesu ameweka wazi ni namna gani waweza kumpenda Yeye, Yohana 14:21 inasema, "Yeye aliye na AMRI  zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye, naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; Nami nitampenda na kujidhihirisha kwake"
 Nayo Mithali 3:1-2 inasema, " Mwanangu, usiisahau sheria yangu, Bali moyo wako uzishike AMRI zangu.Maana zitakuongezea WINGI WA SIKU, NA MIAKA YA UZIMA, NA AMANI"
 Unapozishika sheria na Amri alizozitoa Bwana maishani mwako...huo ndo udhihirisho wa Upendo wako kwa Mungu aliye hai...kila unapoongeza bidii ya kumtii na kumheshimu Mungu-ukakaza kumpenda, ANAKUSHIBISHA KWA SIKU NYINGI...Wewe ndiye unayeweza kumwambia Bwana, hii miaka 90 inatosha, nimekwisha shiba maisha...nataka kurudi nyumbani...au miaka 40 inatosha Bwana...nimeshiba siku nataka kurudi nikae na wewe...wewe ndo unayeamua wingi wa siku zako...tangu leo kaza kumpenda BWANA.
               Ninaamini umejifunza kitu, na ya kuwa wewe nawe utayagusa maisha ya wengine kwa KWELI hizi ambazo Bwana amesema na wewe kupitia kwangu.Ubarikiwe
    Wako katika na Ndani ya Kristo

Kwa Viumbe Vyote Barabara 13


Bwana Ndiye Mchungaji.


Mwili wako ni Hekalu la Mungu!

1 KOR. 6:18-19

Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe. Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe.

Wako wapi mabinti/wakaka wanaomuheshimu MUNGU…Unapopiga picha za utupu na kuweka mitandaoni siyo kwamba unawaburudisha watu la! hasha bali unajishushia thamani wewe. alafu unamkosea MUNGU kwa sababu Mwili wako ni HELAKU,mwili ni Nyumba iliyovaa ROHO…MUNGU alikufinyanga akakutengeneza ili uje Duniani…Yaani wewe asili yako ni MBINGUNI…..Wanadamu wote walitoka mbinguni, na asili yetu ni mbinguni kwa Mungu. Hata ukisoma maandiko yanaelezea vizuri, Yeremia 1:5 “Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa” …Mtu anapoingia katika kitendo cha uzinzi maana yake anachafua HEKALU LA MUNGU..

sio hivyo tu hata kuchana chale ni kosa kubwa, Agano la kale liliwaamuru waIsraeli, “Msiikate miili yenu kwa ajili ya wafu wala kuchanja chale juu ya ngozi za miili yenu.Mimi ni Bwana” (mambo ya walawi 19:28)…Tambua matumizi ya MWILI WAKO….Heshimu mwili wako maana ni HEKALU TAKATIFU
Tunapaswa kufahamu kuwa miili yetu na nafsi zetu pia zimekombolewa na ni mali ya Mungu. Ijapokuwa haelekei moja kwa moja juu ya chale na alama za miili, 1 Wakorintho 6:19 -20 inatupatia kanuni moja, “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu, akaaye ndani yenu, ambaye mnaye kutoka kwa Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe. Mmenunuliwa kwa thamani kwa hivyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu na katika roho zenu ambvyo ni vya Mungu.” Miili yetu sharti iandamane na ukweli kokote tuendako.
–Conrad Conwell.

Mwili wako ni wathamani

Vitu Vyote Vya THAMANI Hapa Duniani, Mungu Ameviweka Mahali Ambako Ili Kuvipata LAZIMA Ufanye Kazi Ya Ziada!
MAFUTA Ni Malighafi Ya Thamani Sana, Yako CHINI SANA Kuyapata Mpaka UCHIMBE CHINI SANA NA KWA GHARAMA... Ndivyo Ilivyo Kwa DHAHABU, ALMASI, TANZANITE Na Madini Yote Ya Thamani!

MWILI WA MWANAMKE Nao Ni KITU CHA THAMANI SANA, Kuliko MAFUTA, AU MADINI YOYOTE Unayoyafahamu Wewe... Ndio Maana Biblia Inasema SISI VIDUME TUKIPATA MKE TUMEPATA KITU CHEMA [Kwanza] LAKINI Pi...a TUNAKUWA TUMEPATA NA KIBALI CHA ZIADA TOKA KWA BWANA, Ambacho Kinakuja Tu UNAPOMPATA MWANAMKE Yaani "KITU CHA THAMANI"
(Soma Mithali 18:22 Ujiionee Hii Siri Ya Ajabu Sana)!

UKIMWONA MTOTO WA KIKE ANAACHA NJE KIUNGO CHOCHOTE CHA MWILI WAKE, Yawe MATITI, TUMBO, KITOVU, SEHEMU ZA MIGUU Nk, Wakati "VITU VIDOGO" KAMA DHAHABU, ALMASI, TANZANITE, MAFUTA Nk Vimefichwa Sana, USIMLAUMU, HUYO HAJUI THAMANI YAKE, HAJUI KUWA YEYE NI KITU CHEMA... HAJUI KUWA MWILI WAKE NI HAZINA YA PEKEE ANAYOPASWA KUISITIRI MPAKA ATAKAPOKUTANISHWA NA KUUNGANISHWA NA MMEWE AMBAYE KWA MUJIBU WA NENO LA MUNGU HUYO PEKEE NDIYE "MWENYE MAMLAKA JUU YA HUO MWILI"

ACHENI KUWAPA FAIDA WANAUME WENGINE, VIUNGO VYAKO MALI YA MMEO BWANA, MTUNZIE YEYE... Linda Heshima Na Utu Wako Eee Mwanamke Na Wewe Mdogo Wangu Uitwaye MSICHANA... Waache Wazungu WAMESHACHANGANYIKIWA NA MMOMONYOKO WA MAADILI WALIOSHINDWA KUUZUIA, WANATAKA KUTUSAMBAZIA SUMU NA SISI... Tushike Viwango Vya Neno La Mungu, Japo MAVAZI SI TIKETI YA KUKUPELEKA MBINGUNI!

Tusizidiwe AKILI Na Hawa Majirani Zetu Wana Wa Ishmaeli Wanaojisitiri Vema Maungo Yao... Ingawa Kweli Ndani Hawako Hivyo!

Wednesday, February 5, 2014

Vuka Historia Yako

Bwana YESU Asifiwe, kwanza nataka ujue kuna watu HISTORIA ya Maisha yao imesimama hapo hapo haiendi mbele wala hairudi Nyuma,Wakati Mwingine hali hii imesababisha hata watu wako wa karibu waone hiyo ni historia yako siku zote..Lakini nataka nikuambie HISTORIA HIYO leo inakwenda kubadilika,Watu wa karibu walimuona yule RAHABU kama ni kahaba aliyeshindikana na hata ndugu walikuwa wanamtegemea yeye na kazi ile ya Ukahaba,Ni kweli Rahabu alikuwa na msaada mkubwa sana kwa ndugu zake,lakini msaada ule ulikuwa na dosari (Shetani ndiye alikuwa anahusika) Rahabu alipochukua hatua ya kumsogelea MUNGU,MUNGU akambadilisha (Yoshua 6:25) “Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu,yule kahaba,na watu wa nyumba ya baba yake,na vitu vyote alivyokuwa navyo naye akakaa kati ya Israel hata leo;kwa sababu aliwaficha wale wajumbe aliowatuma Yoshua ili kuupeleleza mji wa Yeriko”..
Ukiusoma huu mstari kwa umakini utaona Kupitia Rahabu nyumba nzima waliokoka, Biblia inatuambia akakaa kati ya Israel hata leo (Maana yake akahesabiwa ni kizazi cha Israel) Hujanielewa? Ebu soma hapa (Waebrani 11:31) “Kwa imani Rahabu,yule kahaba,hakuangamia pamoja na hao walioasi;kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani” Unaweza ukaona Rahabu alifanya kitu kidogo sana lakini kwa MUNGU ni kikubwa sana…MUNGU akaona vema Amuweke Rahabu katika kundi la wazee wa IMANI (Waebrania 11:39) “Na watu wote hao wakiisha kushuudiwa kwa sababu ya imani yao”
Ebu leo Vuka historia yako “Bwana yu pamoja nawe Ee shujaa (Waamuzi 6:12b) Vuka Historia yako leo,yawezekana una ugonjwa ambao waliumwa Babu/Bibi zako au Baba/Mama zako,yawezekana unahistoria ya kujikaata kuwa wewe haufahi au kuna dhambi umetenda unaona ni vigumu kurudi kwa MUNGU….Sikia nikwambie MUNGU anasamehe..Rudi leo….Rahabu aliporudi kwa MUNGU Historia MPYA ilifunguka katika maisha yake

MAMBO YA MSINGI 20 YA KUJIFUNZA KUTOKA KWA HABARI YA DAUDI NA GOLIATHI 1SAMWELI 17:1-55, NA 18: 1-5.



                                                      
1.JINA LA YESU lina uwezo mkubwa kuliko majina yote. Daudi akasema nakujia kwa Jina la BWANA. Tumia jina hilo unapotaka maombi yako yawe na ushindi. 

2.Mawe matano yanawakilisha huduma tano, uchungaji, utume, unabii, ualimu na uinjilisti. Hawa wote wanatakiwa kuwepo katika kanisa na kulelewa namchungaji ndio maana ya Daudi kuweka mawe hayo ndani ya mkoba wa kichungaji.

3.Daudi alichukua mawe matano pia kwa sababu alipeleleza na kujua Goliathi ana ndugu wengine wanne wenye mwonekano kama wake (THEOLOGY). Katika hili tunajifunza kujipanga kwa changamoto za baadaye hata kama bado hazijafika. Kama leo ni shwari basi jipange kwa ajili ya Kesho. Kwa lugha ya uchumi tunasema jifunze kuweka akiba.

4.Upako wa Kwanza ulimpa Daudi nguvu ya kujihesabia mshindi hata kabla ya watu kujua kuwa yeye ni mshindi. Alitafuta kutumia nguvu yake. Usikae kimya wakati kuna jambo linaharibika na unajua kabisa unao uwezo wa kuweka mambo kwenye mstari.

5.Ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo. Sauli na majeshi ya Israeli walijiona wanyonge na dhaifu kwa Goliathi.(walifadhaika na kuogopa sana) lakini Daudi alijiona kuwa mshindi na kweli akamshinda Goliathi.

6.Daudi alitumia silaha dhaifu (kombea na jiwe) lakini alishinda, maana yake hata kama unahisi huna nguvu nyingi, huna pesa nyingi, huna jina kubwa, huna elimu kubwa, unadharaulika kama Goliathi alivyomdharau Daudi, Mungu akikutia nguvu, kile kidogo ulichonacho kinaweza fanya mambo makubwa saana! Efeso 3:20 Mungu hufanya zaidi hata tuwazayo na tuombayo.

7.Daudi hakutafuta umaarufu, kwa sababu kama angependa umaarufu basi baada ya kuua dubu na simba angejitangaza lakini alitulia mpaka alipokutana na Goliathi. Tena hata baada ya kumuua Goliathi ni wana wa Israel walioanza kumwimbia nyimbo nzuri zaidi ya zile za mfalme. Si yeye aliyejitangaza. Nia yake haikuwa kujulikana bali kufanya mapenzi ya Mungu. Usihubiri au kuimba ili tukujue bali fanya kwa ajili ya ujenzi wa ufalme wa Mungu. Mungu akikuinua hutapata shida ya kujitangaza.

8.Mungu huwainua watu kutoka kiwango kimoja kwenda kingine. Upako mmoja hadi mwingine. Daudi alipomuua simba na dubu ndipo alipoweza kumuua Goliathi. Unapotulia na kunyenyekea chini ya Mkono ulio hodari wa Mungu,basi Yeye atakuinua kwa wakati wake(1Petro 5:6). Muda mwingine Mungu anaonekana kama anachelewa kwa sababu tunataka kuruka hatua, katika maisha yako, Mungu anajua hatua unazotakiwa kupita, ukiisha kuua simba na Dubu Mungu atakuwezesha kumuua Goliathi. Mungu anapotaka kukuinua lazima aruhusu tatizo ambalo wewe peke yako ndo utakuwa na jibu lake.

9.Tunajifunza pia kwamba matatizo siku zote yapo tu haijalishi unafanya kazi gani. Usifikirie kwamba ukiwa mtumishi basi majaribu yanapungua.ooh, mengi tu. Popote ulipo jifunze kuwa mwaminifu na Bwana atakuinua. Daudi alikuwa mwaminifu kwa kuhakikisha usalama wa wanyama malishoni ndipo Mungu akamwamini na kumpa Taifa zima la Israel. Umeshindwa kuongoza familia yako, utawezaje kuendesha kanisa la watu mia? Umeshindwa kuongoza idara ya watu 6 unataka kuwa mkurugenzi wa kampuni ili iweje? Usije sema labda nikioa ndo nitaacha uzinzi, labda nikipata milioni mia ndio nitaacha wizi, au labda nikibadilishiwa kazi ndo nitaacha rushwa. HAPANA, tenda kwa uaminifu hapohapo ulipo na Bwana atakuona.

10.Katika kila jambo, hata kama dunia nzima watasema hili haliwezekani wewe soma LUKA 1:37. “hakuna la kumshinda Mungu” Ndio maana kaka zake walipomkebehi Daudi, yeye hakujali akamfuata Goliathi na kumuua. Vikwazo vya mafanikio yako vinaweza kutokea hata ndani ya familia yako au kwa watu wako wa karibu sana, tena wanaoonekana wenye uwezo kuliko wewe, hakuna sababu ya kukata tamaa ni mwanzo mwisho tunasonga mbele. Umetengwa baada ya kumpokea Yesu? Kaza buti songa mbele mpaka Goliathi atie amri chini.

11.Daudi hakufurahia watu wa Mungu wanapotukanwa. Kama mtu wa Mungu kamwe usifurahie watu wanapomsema mtumishi wa Mungu vibaya, hata kama ni kweli katenda uovu, endapo ni mpakwa mafuta wa Bwana kuna utaratibu wa kuyasema na si kuropoka tu. Kumbuka watu wa karibu ya Musa waliadhibiwa na Mungu kwa sababu walimsema vibaya Musa japokuwa ni kweli alikosea.

12.Vita kati ya wana wa Israeli na wafilisti vinawakilisha vita vya watu wa Mungu dhidi ya Shetani na jeshi lake na imetupasa kulishinda kwa kukaa ndani ya Neno(ujumla wa huduma tano kanisani) na kulitumia Jina la Bwana.

13.Shetani ana mikwara mingi sana. Anatumia ufahamu wetu kutufanya tuhisi kwamba yeye anaweza zaidi yetu. Goliathi alitumia muda mwingi kuwatisha majeshi ya wana wa Israeli, kama ilivyo leo shetani anavyokutisha kwamba hutapona, hutafanikiwa, utakufa, utachekwa ukiokoka nk. Daudi hakutishwa kamwe. Unapoiruhusu roho ya hofu ndani yako basi unafanyika mateka wa Shetani. Tunatakiwa kuangusha ngome za fikra zetu zipate kutii uwezo wa Jina la Bwana badala ya kuogopeshwa na matatizo. Tatizo lako ni la muda mfupi tu amini sasa na Bwana atakutokea na kukushindia.

14.Usijadiliane na adui. Wana wa Israeli walitakiwa kujipanga kuvamia, kwa mfano wangeamua watu sita wamvamie Goliathi na wengine wavamie jeshi la wafilisti wangemaliza kelele zote za Goliathi. Kitendo cha kujadiliana na Goliathi kilimpa Goliathi nafasi ya kuingiza hofu mioyoni mwao, don’t compromise with devil’s deceptions /techniques.

15.Daudi alivaa nguo za kijeshi lakini akavua baada ya kuona hazimfai. Maana yake unaweza kujaribu suluhisho/njia za mtu mwingine lakini haishauriwi kwa sababu Mungu alikuumba wewe original, unapocopy na kupaste maana yake uwezo wako na wajibu wako unauweka kuwa kipolo na ufanisi wako unaweza kuwa na matunda kidogo. Japokuwa unaweza usijue kama matunda yako ni madogo. Usiseme kwa sababu wengi wanasoma sheria au udaktari basi na mimi lazima nisome, usiseme kwa kuwa wengi wanapinga Injili basi na mi naogopa kuwa wa tofauti. Mungu alikuumba ukiwa tofauti kabisa na watu wengine, Mungu huwa hafanyi duplications. Anaumba vitu vipya. Hata mapacha wa kufanana nao wanatofauti kubwa sana. Mungu ana kusudi na maisha yako, tafuta kujua na utende vema.

16.Kuwa na umri mdogo si kigezo cha kukuzuia kufanya mambo makubwa ya ufalme wa Mungu. Daudi alikuwa na miaka 17 wakati anamuua Goliathi. Alikuwa mtoto wa mwisho na aliyedharaulika (katika sura ya 16 mzee Yese hakumuhesabu kati ya watoto wake lakini Samweli alisisitiza kama yuko mwingine ndipo Yese alipoagiza Daudi aitwe kutoka malishoni) lakini alitoa suluhisho la nchi nzima. Jitambue na kuelewa ni hazina gani Mungu ameweka ndani yako! Leo kuna milionea wengi tu ulaya ambao wana umri wa miaka ishirini, hata wewe unaweza kuwa miongoni mwao. Hii ndio sababu sioni ugumu kufundisha na kuandika masomo ya mahusiano, kwa sababu Mungu amenifundisha hata kabla sijaoa.

17.Mtu asiyetahiriwa (asiye na agano la Mungu, yaani mganga wa kienyeji, mchawi, mshirikina, kibaka, mwuaji, na wafananao na hao) hana uwezo wa kuyatisha maisha yako ukimtegemea Kristo.

18.Daudi akasema asizimie moyo mtu yeyote kwa ajili ya huyu, mimi mtumishi wako nitakwenda kupigana na mfilisti huyu. Nami nakuambia leo usizimie moyo kwa ajili ya jambo hilo (Ukosefu wa ajira, ugonjwa, fitina, umasikini nk) maana katika yote tunaye atushindiaye, Kristo atayamulika mapito yako na kukushika kwa mkono wake wa kuume pale tu utakapoamua kumwamini kwa moyo wako wote.

19.Daudi alimkata kichwa Goliathi kwa upanga (Neno la Mungu ni kama upanga). Kwa hiyo hakikisha unapoingia vitani una neno la Mungu la kutosha na unaliweka katika matendo, hata Yesu alipojaribiwa alitumia Neno la Mungu kwa ufasaha na akamshinda shetani.

20.Mfalme Sauli hakumwacha Daudi arudi nyumbani kwake. Unapokuwa mshindi, yaani umeleta suluhisho au kufanya jambo la kipekee sehemu fulan(kanisani, ofisini, idarani, wizarani, ndani ya taasisi nk) lazima heshima yako itapanda tu, bosi atatamani uwe assistant wake, Daudi kutoka malishoni mpaka kuishi ikulu si mchezo. Fanya vizuri sehemu uliyopo ndipo Mungu atakupeleka hatua ya juu zaidi, kuwa mnyenyekevu, mwenye bidii na mcha Mungu. 


BARAKA ZA BWANA

Mwana Kondoo
  "Baraka za Mungu zinapokuja kwa mtu humbadilisha mpaka jina.
Kabla ya baraka aliitwa YAKOBO baada ya baraka akaitwa ISRAEL .Kabla ya baraka aliitwa ABRAHAM Baada ya baraka akaitwa IBRAHIM,
Kabla ya baraka unaitwa MASIKINI ukibaliwa utaitwa TAJIRI.Ombi langu Mungu akupe jina jipya ktk jina la YESU.