Wednesday, November 5, 2014

KWA VIJANA.......

Biblia inasema, "Kumcha Mungu ni kuepuka(kukwepa) uovu" na pia inasema, "Zikimbieni tamaa za ujana" lakini pia inasema, "Ikimbieni zinaa" ....Lakini cha ajabu ni kwamba vijana wengi wanafanya kinyume na Biblia inavyosema, hawakai mbali na mazingira hatarishi yanayoweza kuwapelekea kufanya mambo ya ajabu....Utakuta kijana anaishi room na ma room-mate wanaongea vumbi(pumba) halafu naye anakaa tu...anajisemea moyoni mwake, "Nitasikiliza tu ila sitafanya kama wao" ...Usiwe mpumbavu, Mungu anajua udhaifu ulionao katika mwili wako,ndo maana anasema, "Heri mtu yule...asiyeketi barazani pa wenye mizaha" ...Maneno wanayoyasema yatapanda mbegu fulani,ambayo mwisho wa siku itakomaa na itatoa matunda ambayo hautayapenda...Utakuta mkaka/mdada anaongea na simu (hasa usiku-mida ya xtreme au boom club nk) mpaka simu inakuwa ya moto,inaishiwa chaji,anaichaji na ana 'keep talkin' tangu saa 5 usiku hadi 8usiku,..Muda wote huo anaongea na mtu mmoja...tena wa gender ingine...mnaongea nini 3 consecutive hours?...Najua siku ya hukumu kuna watu wataona hata aibu kusikia maongezi yao...wengine watatoa macho watakapoambiwa wasome sms zao na wengine wataduwaa wakiletewa chat-mail zao...kuna mambo mengi sana mnayoyafanya nyuma ya pazia...mkiwa peke yenu huku Mungu akiwatazama...Self discipline ni ya muhimu sana, we mkaka utakaaje na mdada kwenye 'angle mbaya' mpige story masaa kadhaa...unajua nia ya huo mwili wako? NIA ya Mwili ni Uadui dhidi ya Mungu(Warumi 8:6-7) ...Utakuja kushtuka tayari umefanya vituko...jitahidi ufanye kile Biblia inachosema: Epuka uovu... Zikimbie tamaa za ujana...Ikimbie zinaa...Haisemi OMBA au Funga siku kadhaa!

No comments:

Post a Comment