Tuesday, November 18, 2014

NEEMA YA MUNGU..

 
Tito 2:11..

Neema ni upendeleo (Favour),au Katika tafsiri nyingine Neema ni usaidizi wa Kimungu (Divining Patronage).

Biblia inasema katika Tito 2:11 ( Maana Neema ya Mungu iletayo wokovu imefunuliwa), kufuatana na kitabu cha Tito "kwamba neema ya Mungu iletayo wokovu imefunuliwa, ikiwa na maana hakuna mtu anayeweza kuokoka au kumsogelea Mungu isipokuwa Neema ya ...Mungu imefunuliwa kwake. (Yohana 14:6)

Ukiangalia Yohana 14:6 inasema hakuna awezaye kwenda kwa Baba isipokuwa kupitia Mimi (Yaani Yesu Kristo),kwa lugha nyingine naweza kusema,ukifika mahali pa Kuokoka na kumpenda Yesu ujuwe ya kwamba si wewe,wala si nguvu zako ila ni Neema au usaidizi wa Mungu umekuvuta kwake.

Kwa lugha nyepesi vile ulivyo usijivune,usijigambe,usijiinue,ila Mshukuru Mungu kwa Neema Yake ya kuwa hivyo ulivyo,maana ni upendeleo juu ya Maisha yako.Jiulize umeshasafiri mara ngapi kwa umri uliokuwa nao?, Umeshaziona ajali ngapi kwa macho yako lakini huko salama Mshukuru Mungu maana ni neema yake imekufanya uwe mzima,kila kunapokucha Mshukuru Mungu kwa upendeleo wake.Sasa tuangalie 1Samweli 16:7-13.Utaona namna Mungu anavyojaribu kumfundisha mtumishi wake Samweli kwamba yeye(Mungu) aangalii uso,urefu wala kimo,na cha nyongeza wala elimu ya mtu.Kwa maana nyepesi Mungu avutwi kutuchagua tumtumikie kama watu wanavyochag...ua,yeye anaangalia moyo Pia ujue kwamba kuna kitu kinaitwa satanic grace(yaani neema au upendeleo wa shetani),utakuta mwanaume au kijana amezini na zaidi ya wanawake 50,na anajigamba kwamba atakama hana Hela wanawake wanamkubali tu,na upande wa pili kwa wanawake au wasichana,ujue huyu mtu amechaguliwa na shetani kujenga ufalme wa zinaa duniani,kwa hiyo nakuonya wewe mwenye roho hizo chafu,ujue unatumika kwa faida ya shetani na kwa hasara yako.
Utakuta familia ya watoto watano cha ajabu mikoba ya kichawi inamchagua mmoja,kwa nini? ni kwa sababu kibali cha kichawi kimemchagua mtu huyo,cha kufanya kataa kwa jina la Yesu mambo yote ya ki shetani atakama yanakupa sifa na heshima,shetani anakupenda na kukutumia kwa mapenzi yake then ataku damp(tupa)

BY: BISHOP DEO
(THE BODY OF CHRIST MINISTRY MOROGORO)
0717 660807

MAFANIKIO YAKO YA MWILINI NI MATOKEO YA MAFANIKIO YAKO YA ROHONI

3.YOHAN:1:2
 "Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo."

Shaloom mwana wa MUNGU, ninapenda kushare nawewe kwa ufupi sana somo hili ambalo MUNGU amenipa kwaajili yako.
 Labda wengi wetu tunaweza tukawa tumeshindwa kuelewa connection iliyopo kati ya yale tuyaonayo katika ulimwengu wa mwili na yale yaliyopo katika ulimwengu wa ROHO.
KWA KIFUPI YALE YANAYOTUKIA MWILINI nimuhimu ujue kwamba YALIANZIA ROHONI KWANZA. Hivyo uyaonayo mwilini ni matokeo ya ROHONI.
Na ndiyo maana ukisoma NENO LA MUNGU vizuri katika kitabu cha WAEFESO:6:12, Utaona kuna aina ya vita tunafundishwa namna ya kupigana, SASA MUNGU hataki tuangaike kupigana katika mwili kwa sababu ANAIONA HIYO VITA ULIYO NAYO SOURCE yake ni rohoni na ili TUSHINDE VITA nasisi inatupasa tuingie ROHONI.
Ndugu 3YOH:1:2 Unaiona sasa namna inavyo husianisha mafanikio yako katika kila jambo linalo husu maisha yako na KUFANKIWA KWAKO ROHONI.
Anasema NAOMBA UFANIKIWE KATIKA MAMBO YOTE KAMA ROHO yako ifanikiwavyo, KWAHIYO KAMA HAUJAFANIKIWA ROHONI NI VIGUMU KUFANIKIWA MWILINI, mafanikio ya rohoni HUDHIHILIKA MWILINI.
HIVYO KAMA UNATAKA MUME anza jambo kwanza rohoni, kama unataka kazi anza kwanza rohoni, kama unataka watoto anza kwanza rohoni, kama unataka kufanikiwa masomoni anza kwanza rohoni, FUTURE YAKO NAIONA IPO ROHONI anzia huko utauona ukuu wa BWANA.
UKIONA MTU KAENDA KWA MGANGA anataka afanikiwe kimaisha au apate kazi au awe na mvuto kwa wanaume aolewe JUA KWAMBA ANATENGENEZA ROHONI KWA KICHAWI, kwasababu waganga ni WACHAWI wa kawaida kabisa.
SIKIA MTU WA MUNGU hakuna msaada kwa waganga wa kienyeji KWANZA KABISA WENYEWE HAWANA HAYO MAFANIKIO UNAYO YAHITAJI watakulia fedha zako na kuku zako tu.
LAKINI LIPO TUMANI PALE MSALABANI tunakwenda kufanikiwa rohoni hadi mwilini katika kila jambo kwa jina la YESU
 OMBA NAMI SASA
 BWANA YESU ninakushukuru kwamaana UMENIPA ufahamu mpya juu ya UHUSIANO ULIOPO KATI MAFANIKIO YANGU ya rohoni na mwilini, SASA NIMEAMUA kuanza vita ya rohoni ili nipokee katika mwili, WALE WOTE walio funga mafanikio yangu katika ulimwengu wa roho kwa kichawi, MOTO wa BWANA UWATEKETEZE. KATIKA JINA LIWEZALO LA BWANA YESU KRISTO AMEEEEEEN... UBARIKIWE maana unakwenda kufanikiwa sasa.
N.BAMPELE-0762186639

Wednesday, November 5, 2014

KWA WAOAJI......

MWANANGU MPENDWA NAOMBA UNISIKILIZE KWA UZURI KABLA HUJAOA...

1.Mwanangu.
mwanamke anaweza kuwa mkeo,mwingine anaweza kuwa Mama watoto wako,lakini ukipata mwanamke ambaye atakuwa kama mama kwako,mama kwa wanao na mama kwa familia.tafadhari mwanangu usimuache huyo!

2.Mwanangu
Usimfanye mwanamke wako kuwa ndio wa kupika na kufanya kazi zote za jikoni peke yake,tabia hiyo siyo nzuri kwani hata ...nyakati zetu Mashamba yetu yalijulikana kwa majina yetu wanaume lakini tulifanya kazi pamoja

3.Mwanangu
Nikikwambia wewe ni kichwa cha familia,simaanishi kutuna kwa pochi lako,usiangalie kabisa pochi lako,angalia kama utaona tabasamu usoni kwa mke wako.Pesa sio kila kitu katika ndoa haileti ukuu wa familia!

4.Mwanangu
Ukitaka kuwa na maisha marefu na ukapunguza misongo ya mawazo,ongea na mkeo pangeni bajeti na mahitaji yenu,kasha mwache mkeo awe na jukumu la kuratibu mahitaji ya kila siku ya familia kwa kumkabidhi fungu husika hata kama limetokana na michango yenu wawili..
Wanawake wanajua sana kupanga bajeti na haitakuwa rahisi yeye kutumia hela hovyo,wakati akijuwa nyumbani kuna mahitaji ya msingi,lakini hela zikiwa kwako ataendelea kuomba hata kama utakuwa umeishiwa

5.Mwanangu
Usithubutu kumpiga mkeo,maumivu ya kipigo hukaa ndani ya moyo wake kwa muda mrefu sana na huacha kidonda ambacho hukawia sana kupona.Ni hatari sana kuishi na mwanamke mwenye majeraha moyoni

6.Mwanangu
Sasa unaamua kuoa,kama bado utaendelea kuishi maisha kama ya ubachela na mke wako,sio muda mrefu utakuwa bachela tena.Ukioa badilika anza kuishi maisha ya mke na mume.

7.Mwanangu
Zamani tulikuwa na wake wengi na watoto wengi kwa sababu tulikuwa na mashamba makubwa na mavuno yalikuwa makubwa,lakini kwa sasa maisha yamebadilika,kwa hiyo mkumbatie mwanamke wako peke yake kwani hakuna ardhi tena na mahitaji ya watoto ni makubwa sana.Angalia ukubwa wa familia yako!

8.Mwanangu
chini ya mwembe ambao nilikuwa nikikutana na Mama yako inaweza kuwa ni hoteli kubwa nyakati zetu,lakini kumbuka kitu pekee tulichoweza kufanya chini ya mwembe ilikuwa ni kukumbatiana pekee,Nakushauri ukikutana na marafiki wa kike kikubwa unachoweza kufanya nao ni kupeana mikono na ikizidi ni kukumbatiana hadharani na si vinginevyo.

9.Mwanangu
Usibadilike mara utakapoanza kupata mafanikio zaidi kuliko kuwahudumia hao viruka njia wa mtaani ambao hawajui mmetoka wapi na mkeo nakushauri utumie na kufurahia mafanikio yako na mkeo ambaye aliweza kusimama imara wakati wote wa mapito yenu magumu

10.Mwanangu
Kumbuka unapoanza kusema au kuona mke wako kabadilika,ujue kuwa kuna kitu ambacho ulikuwa unakifanya umekiacha kukifanya.Jitathmini na anza kufanya au kutimiza wajibu wako

11.Mwanangu
Usijaribu kumfananisha au kumlinganisha mke wako na mwanamke mwingine wa nje,kwani hata yeye anakuvumilia sana na hajakufananisha na mwanaume mwingine yoyote huko nje na ndio maana aliamua kuwa na wewe.

12.Mwanangu
Sasa hivi kuna hiki kinaitwa haki za wanawake,ni sawa kama mwanamke anasema ana haki sawa na wewe katika nyumba basi gawanya mahitaji yote ndani kwenu katika sehemu mbili zilizo sawa,halafu timiza nusu yako na mwambie atimize nusu iliyobaki

13.Mwanangu
Nilimuoa Mama yako akiwa bado kigoli (Bikra) na nilikuwa naenda sana kwao kabla sijamuoa,lakini kutomkuta mkeo bikra kusikufanye umalaumu kuwa alikuwa muhuni kumbuka,wanawake wa Enzi zetu na wasasa ni tofauti,ulimchagua mwenyewe, na ukigoli hukuujua kabisa.Usiingize mambo ya kabla ya ndoa kwenye ndoa yenu.

14.Mwanangu
Sikuwapeleka Dada zako shule kwa kuwa nilikuwa njinga kama wazee wengi wa hapa kijijini wasemavyo,tafadhari usifanye ujinga huu,kwani kiwango cha mafanikio ya wanawake wa sasa kimefanya wanaume waonekane ni watu wa kawaida sana na sio muhimu kama Enzi zetu.Ukijaliwa watoto wape elimu.

15.Mwanangu
Zamani Enzi za ujana wetu,wanawake walikuwa na urembo wa asili,ingawa siwezi kukudanganya,wengine waliongeza urembo kwa kujichora hina na hata kutoboa pua na masikio lakini usisahau hawakuonesha maumbile yao na nyeti hadharani

16.Mwanangu
Mama yako na mimi hatuna hisa katika kila kitu kinachoendelea katika maisha yenu,Jaribuni kutatua changamoto zenu wenyewe bila kila mara kuja kwetu kuomba usuluhishi.Ndoa ni pamoja na ukomavu wa kutatua changamoto zenu bila kuziuza kama gazetini kwa kila mtu.

17.Mwanangu..
Nilimnunulia mama yako kifaa cha kupikia vitumbua ili aanzishe mradi wa kuuza vitumbua,pia nilimsaidia kununua cherehani yake ya kwanza,Tafadhari msaidie mke wako kutimiza ndoto zake kulingana na uwezo wako kama ambavyo unahangaika kutimiza ndoto zako

18.Mwanangu usiache kutusaidia mimi na mama yako,utu uzima una changamoto nyingi sana na Mungu akikujalia utaziona muda ukifika.Pamoja na kutimiza majukumu yako kama Baba wa familia kumbuka pia bado tunaishi na wewe ni motto wetu.

19.Mwanangu...
Kila upatapo muda wa kuomba,omba na familia yako,kuna kesho ambayo huijui,ongea na MUNGU wako ambae anajua kila kitu kila siku

20.NAKUTAKIA MAISHA MEMA YA NDOA MWANANGU NAKUPENDA

KWA VIJANA.......

Biblia inasema, "Kumcha Mungu ni kuepuka(kukwepa) uovu" na pia inasema, "Zikimbieni tamaa za ujana" lakini pia inasema, "Ikimbieni zinaa" ....Lakini cha ajabu ni kwamba vijana wengi wanafanya kinyume na Biblia inavyosema, hawakai mbali na mazingira hatarishi yanayoweza kuwapelekea kufanya mambo ya ajabu....Utakuta kijana anaishi room na ma room-mate wanaongea vumbi(pumba) halafu naye anakaa tu...anajisemea moyoni mwake, "Nitasikiliza tu ila sitafanya kama wao" ...Usiwe mpumbavu, Mungu anajua udhaifu ulionao katika mwili wako,ndo maana anasema, "Heri mtu yule...asiyeketi barazani pa wenye mizaha" ...Maneno wanayoyasema yatapanda mbegu fulani,ambayo mwisho wa siku itakomaa na itatoa matunda ambayo hautayapenda...Utakuta mkaka/mdada anaongea na simu (hasa usiku-mida ya xtreme au boom club nk) mpaka simu inakuwa ya moto,inaishiwa chaji,anaichaji na ana 'keep talkin' tangu saa 5 usiku hadi 8usiku,..Muda wote huo anaongea na mtu mmoja...tena wa gender ingine...mnaongea nini 3 consecutive hours?...Najua siku ya hukumu kuna watu wataona hata aibu kusikia maongezi yao...wengine watatoa macho watakapoambiwa wasome sms zao na wengine wataduwaa wakiletewa chat-mail zao...kuna mambo mengi sana mnayoyafanya nyuma ya pazia...mkiwa peke yenu huku Mungu akiwatazama...Self discipline ni ya muhimu sana, we mkaka utakaaje na mdada kwenye 'angle mbaya' mpige story masaa kadhaa...unajua nia ya huo mwili wako? NIA ya Mwili ni Uadui dhidi ya Mungu(Warumi 8:6-7) ...Utakuja kushtuka tayari umefanya vituko...jitahidi ufanye kile Biblia inachosema: Epuka uovu... Zikimbie tamaa za ujana...Ikimbie zinaa...Haisemi OMBA au Funga siku kadhaa!

MTEGO WA MWINDAJI

Zaburi:91:3’’Maana yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji,..’’
Namshukuru MUNGU aliye nipa kibari cha kushiriki na wewe somo hili la MTEGO WA MWINDAJI, ambalo naamini linakwenda kukusogeza hatua nyingine kabisa katika imani yako.
KIKAWAIDA MTU UNAPO SEMA KWAMBA umeokoka yani umejiunga na uzao mteule wa mwanakondoo, MOJA KWA MOJA huwa unakuwa umetangaza uadui na UFALME WA GIZA.

Hiv...yo acha nikuite kuwa wewe ni mwana vita au mpiganaji au mpambanaji(ni mwanajeshi wa jeshi la mwana kondoo). WAEFESO:6:12 ‘’Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu na roho’’. HAPO UNAWEZA GUNDUA KITU KUMBE WEWE NI MTU wa mashindano LAKINI hayo mashindano hayapo juu ya DAMU na NYAMA, yapo katika ULIMWENGU wa roho, HIVYO kama mkristo ni muhimu uwe na uwelewa wa ULIMWENGU wa roho ili uweze KUPAPAMBANA vilivyo la sivyo UNAWEZA UKAPIGWA NA ADUI.

Sasa twende kwenye somo letu rasmi, MTEGO WA MWINDAJI: Hapa kwanza kabisa na mzungumzia MWINDAJI pamoja na mtego alio utega kwaajili ya anacho kiwinda(anaye windwa). Lakini pia tumwangalie na MWOKOZI(Anaye okoa) wa hii mitego iliyo tegwa na mwindaji.
Katika kufuatilia kwangu nimegundua ya kwamba TUNA WAKRISTO wengi makanisani wanaohudhulia ibada vizuri sana, na niwatoaji wazuri sana wa mafungu ya kumi, LAKINI WAKRISTO wengi wana fikiliaga kwamba kuitwa mkristo peke yake inatosha, WANASAHAU yakuwa adui(SHETANI) Huwa bado anaandaa mitego ya kuwatoa kwenye imani walizo nazo, 1PETRO:5:8 ‘’ Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.’’

Unaona sasa kumbe bado kuna mtu anatafutwa ili amezwe, sasa hapa unaona kutokana na mawindo ya SHETANI anafananishwa na SIMBA aungurumaye akitafuta mtu ammeze, hivyo yupo mawindoni, yeye hali swala, nyati wala punda milia, ndiyo utofauti ulipo hapa wa huyu mfano wa simba, yani yeye chakula chake ni watu tu. So anaweza akakumeza wewe au mimi TAKE CARE.
TUNA MZUNGUMZIA SHETANI kama mwindaji sasa, ambaye ametega mitego yakutosha kwa ajili yako, ili akurudishe nyuma kiimani, aivunje ndoa yako, akurudishe nyuma kiuchumi n.k

Labda acha nikupe kitu kidogo kinacho weza kukusaidia juu ya mwindaji. SHETANI mawindo yake hayakuanza leo, alianza tangu pale EDENI, alimuwinda ADAM kwa muda mrefu ili amtoe kwenye kusudi la MUNGU, na kuuharibu uhusiano uliopo kati ya ADAMU na MUNGU. Aliubadilisha UKWELI kuwa UONGO ili tu ADAMU aingie mtegoni, na kweli alifanikiwa katika hilo. Soma MWANZO:3

NOTE:SI KILA JAMBO LIJALO KAMA BARAKA, NI LAKULIKUMBATIA NA KULIONA LA FAA SANA; MAMBO MENGINE YAMEKUJA KAMA BARAKA KWETU LAKINI NI MTEGO HALISI WA MWINDAJI.
Nimeona watu wengi kutokana na hali ambazo wamekuwa wakizipitia katika maisha yao wamejikuta wakinaswa na mtego wa mwindaji, wengine ni kweli walisimama kiimani lakini walisahau ya kuwa bado walikuwa wanawindwa na mwisho wake ukawa nikuangukia katika mtego wa mwindaji.
NIOMBI LANGU KWA MUNGU AKAITEGUE MITEGO YOTE ILIYO TEGWA DHIDI YA KILA ENEO LINALO HUSU MAISHA YAKO KATIKA JINA LA YESU KRISTO ALIYE HAI.

Naomba nikukumbushe kitu mwana wa MUNGU, shetani hajakutega katika hii leo yako unayoiona ni ya baraka kwako au ni ya furaha kwako, LAKINI NAUONA mtego alioutega kwa ajili yako ni KWAAJILI YA KESHO yako, maana amekutazama akagundua kwamba wewe ni mtu watofauti sana, na mwenye impact(matokeo) kubwa sana kwa wakati ujao wa maisha yako, KWAHIYO NI MUHIMU KUJUA KWAMBA taabu unayoipata leo ni matiokeo ya mtego uliowahi kutegwa na ukategeka kwa wakati huo ulio pita.

HEBU tusogee mbele zaidi sasa. 1Samweli:18:21 ‘’ Naye Sauli akasema moyoni, Mimi nitamwoza huyu, awe mtego kwake, tena mkono wa wafilisti uwe juu yake.’’
Hapa sasa unaweza kuona sasa kumbe kunawatu wana ndoa zilizo mitego kwao, Hapa utamwona SAULI anamwozesha binti yake kwa DAUDI si kwamba awe mke bali awe mtego kwa kwa DAUDI. Anhaa.. Kumbe MUWINDAJI anaweza akakuletea mume/mke ambaye ulikuwa ukimwomba MUNGU kwa muda mrefu, nawewe ukajipa moyo kwamba tayali MUNGU amejibu maombi yako, kuumbee ni MUWINDAJI amekuletea mfano wa mume/mke ili apate kukuingiza au kukunasa mtegoni, HATAKAMA UTASUBIRI KWA MUDA GANI JUA KWAMBA MUNGU NDIYE ATAKAYE KUPA MWENZA WAKO, JIANGALIE USIJE ANGUKIA MIKONONI MWA WANYANG’ANYI..