Tuesday, November 18, 2014

MAFANIKIO YAKO YA MWILINI NI MATOKEO YA MAFANIKIO YAKO YA ROHONI

3.YOHAN:1:2
 "Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo."

Shaloom mwana wa MUNGU, ninapenda kushare nawewe kwa ufupi sana somo hili ambalo MUNGU amenipa kwaajili yako.
 Labda wengi wetu tunaweza tukawa tumeshindwa kuelewa connection iliyopo kati ya yale tuyaonayo katika ulimwengu wa mwili na yale yaliyopo katika ulimwengu wa ROHO.
KWA KIFUPI YALE YANAYOTUKIA MWILINI nimuhimu ujue kwamba YALIANZIA ROHONI KWANZA. Hivyo uyaonayo mwilini ni matokeo ya ROHONI.
Na ndiyo maana ukisoma NENO LA MUNGU vizuri katika kitabu cha WAEFESO:6:12, Utaona kuna aina ya vita tunafundishwa namna ya kupigana, SASA MUNGU hataki tuangaike kupigana katika mwili kwa sababu ANAIONA HIYO VITA ULIYO NAYO SOURCE yake ni rohoni na ili TUSHINDE VITA nasisi inatupasa tuingie ROHONI.
Ndugu 3YOH:1:2 Unaiona sasa namna inavyo husianisha mafanikio yako katika kila jambo linalo husu maisha yako na KUFANKIWA KWAKO ROHONI.
Anasema NAOMBA UFANIKIWE KATIKA MAMBO YOTE KAMA ROHO yako ifanikiwavyo, KWAHIYO KAMA HAUJAFANIKIWA ROHONI NI VIGUMU KUFANIKIWA MWILINI, mafanikio ya rohoni HUDHIHILIKA MWILINI.
HIVYO KAMA UNATAKA MUME anza jambo kwanza rohoni, kama unataka kazi anza kwanza rohoni, kama unataka watoto anza kwanza rohoni, kama unataka kufanikiwa masomoni anza kwanza rohoni, FUTURE YAKO NAIONA IPO ROHONI anzia huko utauona ukuu wa BWANA.
UKIONA MTU KAENDA KWA MGANGA anataka afanikiwe kimaisha au apate kazi au awe na mvuto kwa wanaume aolewe JUA KWAMBA ANATENGENEZA ROHONI KWA KICHAWI, kwasababu waganga ni WACHAWI wa kawaida kabisa.
SIKIA MTU WA MUNGU hakuna msaada kwa waganga wa kienyeji KWANZA KABISA WENYEWE HAWANA HAYO MAFANIKIO UNAYO YAHITAJI watakulia fedha zako na kuku zako tu.
LAKINI LIPO TUMANI PALE MSALABANI tunakwenda kufanikiwa rohoni hadi mwilini katika kila jambo kwa jina la YESU
 OMBA NAMI SASA
 BWANA YESU ninakushukuru kwamaana UMENIPA ufahamu mpya juu ya UHUSIANO ULIOPO KATI MAFANIKIO YANGU ya rohoni na mwilini, SASA NIMEAMUA kuanza vita ya rohoni ili nipokee katika mwili, WALE WOTE walio funga mafanikio yangu katika ulimwengu wa roho kwa kichawi, MOTO wa BWANA UWATEKETEZE. KATIKA JINA LIWEZALO LA BWANA YESU KRISTO AMEEEEEEN... UBARIKIWE maana unakwenda kufanikiwa sasa.
N.BAMPELE-0762186639

1 comment: