Friday, February 7, 2014

Mwili wako ni Hekalu la Mungu!

1 KOR. 6:18-19

Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe. Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe.

Wako wapi mabinti/wakaka wanaomuheshimu MUNGU…Unapopiga picha za utupu na kuweka mitandaoni siyo kwamba unawaburudisha watu la! hasha bali unajishushia thamani wewe. alafu unamkosea MUNGU kwa sababu Mwili wako ni HELAKU,mwili ni Nyumba iliyovaa ROHO…MUNGU alikufinyanga akakutengeneza ili uje Duniani…Yaani wewe asili yako ni MBINGUNI…..Wanadamu wote walitoka mbinguni, na asili yetu ni mbinguni kwa Mungu. Hata ukisoma maandiko yanaelezea vizuri, Yeremia 1:5 “Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa” …Mtu anapoingia katika kitendo cha uzinzi maana yake anachafua HEKALU LA MUNGU..

sio hivyo tu hata kuchana chale ni kosa kubwa, Agano la kale liliwaamuru waIsraeli, “Msiikate miili yenu kwa ajili ya wafu wala kuchanja chale juu ya ngozi za miili yenu.Mimi ni Bwana” (mambo ya walawi 19:28)…Tambua matumizi ya MWILI WAKO….Heshimu mwili wako maana ni HEKALU TAKATIFU
Tunapaswa kufahamu kuwa miili yetu na nafsi zetu pia zimekombolewa na ni mali ya Mungu. Ijapokuwa haelekei moja kwa moja juu ya chale na alama za miili, 1 Wakorintho 6:19 -20 inatupatia kanuni moja, “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu, akaaye ndani yenu, ambaye mnaye kutoka kwa Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe. Mmenunuliwa kwa thamani kwa hivyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu na katika roho zenu ambvyo ni vya Mungu.” Miili yetu sharti iandamane na ukweli kokote tuendako.
–Conrad Conwell.

No comments:

Post a Comment