Wednesday, February 5, 2014

Vuka Historia Yako

Bwana YESU Asifiwe, kwanza nataka ujue kuna watu HISTORIA ya Maisha yao imesimama hapo hapo haiendi mbele wala hairudi Nyuma,Wakati Mwingine hali hii imesababisha hata watu wako wa karibu waone hiyo ni historia yako siku zote..Lakini nataka nikuambie HISTORIA HIYO leo inakwenda kubadilika,Watu wa karibu walimuona yule RAHABU kama ni kahaba aliyeshindikana na hata ndugu walikuwa wanamtegemea yeye na kazi ile ya Ukahaba,Ni kweli Rahabu alikuwa na msaada mkubwa sana kwa ndugu zake,lakini msaada ule ulikuwa na dosari (Shetani ndiye alikuwa anahusika) Rahabu alipochukua hatua ya kumsogelea MUNGU,MUNGU akambadilisha (Yoshua 6:25) “Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu,yule kahaba,na watu wa nyumba ya baba yake,na vitu vyote alivyokuwa navyo naye akakaa kati ya Israel hata leo;kwa sababu aliwaficha wale wajumbe aliowatuma Yoshua ili kuupeleleza mji wa Yeriko”..
Ukiusoma huu mstari kwa umakini utaona Kupitia Rahabu nyumba nzima waliokoka, Biblia inatuambia akakaa kati ya Israel hata leo (Maana yake akahesabiwa ni kizazi cha Israel) Hujanielewa? Ebu soma hapa (Waebrani 11:31) “Kwa imani Rahabu,yule kahaba,hakuangamia pamoja na hao walioasi;kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani” Unaweza ukaona Rahabu alifanya kitu kidogo sana lakini kwa MUNGU ni kikubwa sana…MUNGU akaona vema Amuweke Rahabu katika kundi la wazee wa IMANI (Waebrania 11:39) “Na watu wote hao wakiisha kushuudiwa kwa sababu ya imani yao”
Ebu leo Vuka historia yako “Bwana yu pamoja nawe Ee shujaa (Waamuzi 6:12b) Vuka Historia yako leo,yawezekana una ugonjwa ambao waliumwa Babu/Bibi zako au Baba/Mama zako,yawezekana unahistoria ya kujikaata kuwa wewe haufahi au kuna dhambi umetenda unaona ni vigumu kurudi kwa MUNGU….Sikia nikwambie MUNGU anasamehe..Rudi leo….Rahabu aliporudi kwa MUNGU Historia MPYA ilifunguka katika maisha yake

No comments:

Post a Comment