Tuesday, November 18, 2014

NEEMA YA MUNGU..

 
Tito 2:11..

Neema ni upendeleo (Favour),au Katika tafsiri nyingine Neema ni usaidizi wa Kimungu (Divining Patronage).

Biblia inasema katika Tito 2:11 ( Maana Neema ya Mungu iletayo wokovu imefunuliwa), kufuatana na kitabu cha Tito "kwamba neema ya Mungu iletayo wokovu imefunuliwa, ikiwa na maana hakuna mtu anayeweza kuokoka au kumsogelea Mungu isipokuwa Neema ya ...Mungu imefunuliwa kwake. (Yohana 14:6)

Ukiangalia Yohana 14:6 inasema hakuna awezaye kwenda kwa Baba isipokuwa kupitia Mimi (Yaani Yesu Kristo),kwa lugha nyingine naweza kusema,ukifika mahali pa Kuokoka na kumpenda Yesu ujuwe ya kwamba si wewe,wala si nguvu zako ila ni Neema au usaidizi wa Mungu umekuvuta kwake.

Kwa lugha nyepesi vile ulivyo usijivune,usijigambe,usijiinue,ila Mshukuru Mungu kwa Neema Yake ya kuwa hivyo ulivyo,maana ni upendeleo juu ya Maisha yako.Jiulize umeshasafiri mara ngapi kwa umri uliokuwa nao?, Umeshaziona ajali ngapi kwa macho yako lakini huko salama Mshukuru Mungu maana ni neema yake imekufanya uwe mzima,kila kunapokucha Mshukuru Mungu kwa upendeleo wake.Sasa tuangalie 1Samweli 16:7-13.Utaona namna Mungu anavyojaribu kumfundisha mtumishi wake Samweli kwamba yeye(Mungu) aangalii uso,urefu wala kimo,na cha nyongeza wala elimu ya mtu.Kwa maana nyepesi Mungu avutwi kutuchagua tumtumikie kama watu wanavyochag...ua,yeye anaangalia moyo Pia ujue kwamba kuna kitu kinaitwa satanic grace(yaani neema au upendeleo wa shetani),utakuta mwanaume au kijana amezini na zaidi ya wanawake 50,na anajigamba kwamba atakama hana Hela wanawake wanamkubali tu,na upande wa pili kwa wanawake au wasichana,ujue huyu mtu amechaguliwa na shetani kujenga ufalme wa zinaa duniani,kwa hiyo nakuonya wewe mwenye roho hizo chafu,ujue unatumika kwa faida ya shetani na kwa hasara yako.
Utakuta familia ya watoto watano cha ajabu mikoba ya kichawi inamchagua mmoja,kwa nini? ni kwa sababu kibali cha kichawi kimemchagua mtu huyo,cha kufanya kataa kwa jina la Yesu mambo yote ya ki shetani atakama yanakupa sifa na heshima,shetani anakupenda na kukutumia kwa mapenzi yake then ataku damp(tupa)

BY: BISHOP DEO
(THE BODY OF CHRIST MINISTRY MOROGORO)
0717 660807

No comments:

Post a Comment